Tuesday, March 8, 2016

POLISI WATAKIWA KUTOA HUDUMA BORA KWA MTEJA.


 Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro (SACP) Ulrich Matei, akitoa neno mbele ya washiriki wa mkutano mkuu wa URA SACCOS (hawapo pichani) wakati akifungua mkutano huo wa siku mbili wa chama cha ushirika cha kuweka akiba na mikopo, unaofanyika mkoani Morogoro.
 Washiriki wa chama cha ushirika cha kuweka akiba na mikopo URA SACCOS Wakiimba wimbo wa maadili  kabla ya ufunguzi wa mkutano mkuu  wa siku mbili unaofanyika mkoani Morogoro.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro (SACP) Ulrich Matei, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa mkutano mkuu wa Chama cha Ushirika cha Kuweka Akiba na Mikopo (URA SACCOS) mara baada ya kufungua rasmi mkutano huo wa siku mbili unaofanyika mkoani morogoro huku ukiwashirikisha askari polisi kutoka mikoa yote Tanzania bara na visiwani.(Picha na Demetrius Njimbwi wa Jeshi la Polisi)

No comments: