Tuesday, March 8, 2016

Wizara ya habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo kuendelea kushirikiana na kampuni ya UK sport.

Waziri wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye(kulia) akizungumza na mshauri wa maendeleo ya kimataifa wa kampuni ya Uk sport Bi.Clare Barell juu ya miradi mbalimbali ya maendeleo ya michezo na kumuomba mwakilishi uyo kuwekeza kupitia kampuni yao katika miundombinu ya michezo hapa nchini.
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel akizungumza jambo na mshauri wa maendeleo ya kimataifa wa kampuni ya Uk sport Bi.Clare Barell.Kampuni iyo ni mshirika wa Tanzania katika maendeleo ya Michezo.
Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Prof.Elisante Ole Gabriel(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na mshauri wa maendeleo ya kimataifa wa kampuni ya Uk sport Bi.Clare Barell(wa pili kushoto) alipomtembelea ofisini kwake.Wengine pichani ni Kaimu mkurugenzi Maendeleo ya Michezo Bw.Alex Nkenyenge(wa pili kulia).

No comments: