Wakimbizi kutoka nchini Burundi walioko katika
kambi ya Nyarugusu wakiwa wamebeba shehena ya unga wa mahindi jana,
muda mfupi baada ya kugawiwa chakula hicho Shirika la Umoja wa Mataifa
linaloshughulikia chakula (WFP), lililoweka kituo chake katika kambi
ya wakimbizi ya Nyarugusu wilayani Kasulu, mkoani
Kigoma.
Byesige Josephat (anayemimina mafuta) na Hezron
Mtangirwa(kushoto), wakimbizi kutoka Burundi waliohifadhiwa katika
kambi ya Wakimbizi ya Nyarugusu wakipima mafuta ili waweze kuyagawa
kwa wakimbizi wenzao jana ,baada ya kugawiwa mafuta na Shirika la
Umoja wa Mataifa, linaloshughulikia chakula (WFP), ambalo lina kituo
chake katika kambi ya Nyarugusu iliyoko wilayani Kasulu mkoani
Kigoma.
Kinamama wakimbizi toka Burundi wakipata mgao wao wa
unga unaotolewa kwa wakimbizi wanaohifadhiwa katika Kambi ya wakimbizi
ya Nyarugusu iliyoko wilayani Kasulu mkoani
Kigoma. Serikali kwa kushirikiana na Mashirika ya Kimataifa
imeendelea kuhakikisha kuwa wakimbizi hawa toka Burundi wanapata
chakula cha kutosha kwa ajili ya mahitaji
yao.
Mkimbizi Irene Ntibelenda (katikati) akiwa pamoja na ndugu
yake Sengiyu Mvajeme (kulia) baada ya kupokea mgao wa chakula
unaotolewa na Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia
chakula (WFP), lililo na Kituo chake katika kambi ya
Nyarugusu iliyopo wilayani Kasulu, mkoani Kigoma. Kushoto ni mtoto
wake aitwaye Nsengiyumva
Idiphonce.
No comments:
Post a Comment