Tuesday, September 15, 2015

SHIDA YA MAJI ITEZI UYOLE JIJINI MBEYA.

Kamera Mani wa Globu ya Jamii aliangazia maeneo ya Itezi Uyole Jijini Mbeya na kushuhudia jinsi hali ilivyo katika upatikanaji wa Maji ulivyo kuwa ni washida sana katika maeneo hayo ya Itezi Jijini Mbeya, kama waonekanavyo hapo baadhi ya Wananchi na Wakazi wa Itezi wakiwa katika Sehemu moja wanayo itegemea kwa kutoa huduma ya Maji katika Eneo hilo, Wakazi wa Itezi walipo kuwa wakizungumza na Globu ya Jamii juu ya hali hiyo walisema kuwa hali hii imekuwa Ikiwasumbua kwa muda mrefu kutokana na kukatika kwa Maji mara kwa mara na kwa muda mrefu katika Eneo hilo na kupelekea Watu kutoka Maeneo mbalimbali Sanjari na Eneo hilo kukutana kwa Pamoja katika Kisima Kinacho wapatia Maji kuajili ya shughuli mbalimbali za Kijamii.
Wakina Mama Sanjari na Vyombo vyao vya kuchotea Maji wakiwa njiani kwenda kuteka Maji.
Baadhi ya Vijana Mabinti wa Mtaa wa Itezi Uyole Jijini Mbeya wakiwa wamejitwika Maji kupeleka Majumbani kwao kuajili ya kuendelea na shughuli mbalimvali za Kijamii Majumbani kwao.
Mtoto huyu nae katika Taswira akisukuma Toroli kwenda kuteka Maji.

No comments: