Wednesday, September 16, 2015

MBEYA CITY YAIFUNGA JKT RUVU 3-0 KATIKA MTANANGE WA LIGI KUU YA VODACOM TANZANIA BARA..

Kocha wa Timu ya Mbeya City fc a.k.a Wakoma Kumwanya ndugu, Juma Mwambusi akizungumza jambo na baadhi ya Vyombo vya Habari mara baada ya Mtanange huo wa Ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara kumalizika katika Uwanja wa kumbukumbu Sokoine Jijini Mbeya, Ambapo Mbeya City fc waliibuka kidedea kwa kuichalaza Jkt Ruvu goli 3-0, ambapo Dakika ya 23 mchezaji Joseph Mahundi kuipatia Mbeya City Goli la Kwanza na Goli la Pili toka kwa Temy Felix Dakika ya 57 kwa mkwaju wa Penati, huku Goli la Tatu kufungwa na David Kabole Dakika ya 71.
kiungo wa Mbeya City fc Geofrey Mlawa akiteleza na Mpira katika Mtanange huo uliochezwa katika Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya.
Kamati ya Ufundi..
Baadhi ya Mashabiki Kinazi wa Timu ya Mbeya City fc wakishangilia katika Mtanange huo wa Ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara, ambapo Mbeya City waliibuka mshindi kwa goli 3-0...
Kikosi cha Jkt Ruvu..
Kikosi Cha Mbeya city..



 
Makamera mani wakitafuta Taswirazz...

Kocha wa Jkt Ruvu Fredi Felix akizungumza na Vyombo vya Habari.
Wachambuzi mahiri wa Soka toka Radio Dream fm 91.3 Mbeya, Aplina Philipo Zeze Sanjari na Mkongwe wa Radio Tanzania Tom Chilala walipo kuwa wakirusha laivu Mtanange huo moja kwa moja toka Sokoine Jijini Mbeya.

No comments: