Sunday, April 12, 2015

NAIBU WAZIRI NISHATI NA MADINI ATEMBELEA MGODI WA DHAHABU BULYANHULU.

Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Kitwanga (kushoto) akipeana mkono na Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya uchimbaji madini ya Acacia, Brad Gordon, wakati alipowasili kutembelea mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu, ulioko wilaya ya Msalala mkoani Shinyanga, Jumamosi Aprili 11, 2015.

Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Kitwanga (aliyesimama) akitoa hotuba yake mwanzoni mwa ziara yake ya kutembelea mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu ulioko wilaya ya Msalala, mkoani Shinyanga, Jumamosi Aprili 11, 2015. Kushoto ni Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya uchimbaji madini ya Acacia, Brad Gordon, na kulia ni makamu wa rais wa kampuni hiyo anayeshughulikia masuala ya kampuni hapa Tanzania, Deo Mwanyika.

Kaimu Meneja Mkuu mgodi wa Dhahabu wa Bulyanhulu ulioko wilaya ya Msalala, mkoani Shinyanga, Benedict Busunzu, akizungumza shughuli za uchimbaji madini za mgodi huo na huduma zitolewazo kwa jamii, wakati naibu waziri wa jishati na madini, Charles Kitwanga, alipofanya ziara ya kutembelea mgodi huo, Jumamosi Aprili 11, 2015.
Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya uchimbaji madini ya Acacia, Brad Gordon, akizungumza wakati wa uwasilishaji shughuli mbalimbali zifanywazo na migodi inayomilikiwa na kampuni hiyo hapa nchini ya Bulyanhulu, North Mara na Buzwagi, wakati wa ziara ya naibu waziri wa nishati na madini, Charles Kitwanga, alipotembelea mgodi wa Bulyanhulu uliko wilaya ya Msalala mkoani Shinyanga, Jumamosi Aprili 11, 2015.
Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya uchimbaji madini ya Acacia, Brad Gordon, (wapili kushoto), akimpa maelezo Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Kitwanga, (watatu kushoto), alipotembelea eneo la chini ya ardhi la mgodiwa Bulyanhulu kiasi cha kilomita 1.5 chini ya bardhi, Jumamosi Aprili 11, 2015. Kushoto ni mwenyekiti wa kampiuni ya uchimbaji dhahabu ya Mlalo, Mohammed Hussein.
Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya uchimbaji madini ya Acacia, Brad Gordon, (Kulia), akikabidhi mfano wa hundi ya shilingi milioni 749.53, Afisa Mipango wa Halmashauri ya wilaya ya Msalala mkoani Shjinyanga, Mophen Mwakajonga, ikiwa ni kodi ya huduma (service levy), huku Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Kitwanga (katikati) akishuhudia. Hafla hiyo ilifanyika kwenye mgodi wa Bulyanhulu ulioko wilayani humo April 11, 2015.
Sehemu ya Ujumbe ulioambatana na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Kitwanga katika ziara ya mgodi wa Bulyanhulu April 11, 2015.
Naibu waziri wa nishati na madini, Charles Kitwanga, (wakwanza kushoto) na ujumbe wake, wakipatiwa maelezo ya kiusalama muda mfupi kabla ya kuanza ziara ya kutembelea shughuli za uchimbaji madini chini ya ardhi kwenye mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu uliko wilaya ya Msalala mkoani Shinyanga Jumamosi Aprili 11, 2015.
Naibu waziri wa nishati na madini, Charles Kitwanga, (kushoto), na Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya uchimbaji madini ya Acacia, Brad Gordon, (kulia), wakimsikiliza mtaalam wa shughuli za uchimbaji madini ardhini, wa mgodi huo, wakati wa ziara ya naibu waziri Jumamosi Aprili 11, 2015.

No comments: