Sunday, April 12, 2015

MBOWE AKABIDHI AMBULANCE MBILI KWA HOSPITALI YA WILAYA YA HAI NA HOSPITALI YA MACHAME.

Magari ya wagonjwa yaliyotolewa na Mbunge wa Jimbo la Hai kwa ajili ya wagonjwa jimboni humo.
Mbunge Mbowe akiwa amembeba moja ya watoto waliofika uwanjani hapo kwa ajili ya kushuhudia msaada wa magari ya wagonjwa yaliyotolewa na mbunge huyo kwa watu wa jimbo la Hai.
Muonekano wa ndani wa magari hayo ya kubebea wagonjwa .
Baadhi ya viongozi mbalimbali waliohudhuria shighuli ya makabidhiano iliyofanyika katika uwanja wa Kuni ,Bomang'ombe wilayani Hai.
Wananchi wakiwa wamezingira magari hayo wakiyatizama kwa karibu.
Mbunge wa jimbo la Hai ,akiuzungumza juu ya msaada huo kwa watu wa jimbo la Hai.
Mbunge wa jimbo la Hai,Freeman Mbowe akikabidhi nyaraka mbalimbali za magari hayo kwa Baba Mchungaji Asanterabi Swai ambaye pia ni mkuu wa jimbo kwa niaba ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheli Tanzania (KKKT).
Mmoja wa viongozi wa Machame Hospital ,Swai akifurahia msaada wa gari hilo la wagonjwa kwa hosptali yake.
Mbunge wa jimbo la Hai,Freeman Mbowe akikabidhi funguo wa gari kwa mganga mkuu wa wilaya ya Hai,Dkt Paul Chawote ,msada uliotolewa kwa ajili ya hosptali ya wilaya ya Hai.
Watumishi wa hosptali ya wilaya ya Hai,wakiondoka katika viwanja hivyo mara baada ya kukabidhiwa gari hilo.
Wananchi wakifurahia msaada huo.
Baadhi ya wananchi waliofika kushuhudia makabidhiano ya msaada huo wa magari ya kubebea wagonjwa.
Mbunge wa Jimbo la Hai ,Freeeman Mbowe akizungumza na wananchi mara baada ya kukabidhi msaada wa magari mawili ya kubebea wagonjwa.

Na Dixon Busagaga wa Globu 

ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

No comments: