Wednesday, January 21, 2015

WAFANYAKAZI WA VODACOM TANZANIA WAPEWA ELIMU JUU YA HAKI ZA JINSIA.

Mfanyakazi wa Vodacom Tanzania Esther Mattle akimuuliza swali Mkaguzi Msaidizi wa Jeshi la Polisi Dawati la Jinsia Mkoa wa Kinondoni, Inspekta Prisca Komba, wakati wa semina ya masuala ya jinsia iliyoandaliwa na kampuni hiyo kwa ajili ya wafanyakazi iliyofanyika Mlimani City jijini Dar es Salaam leo.
Baadhi ya wafanyakazi wa Vodacom Tanzania wakifuatilia mafunzo ya masuala ya jinsia yaliyokuwa yakitolewa kwa wafanyakazi wa kampuni hiyo Mlimani City jijini Dar es Salaam leo na Mkaguzi Msaidizi wa Jeshi la Polisi Dawati la Jinsia Mkoa wa Kinondoni, Inspekta Prisca Komba (hayupo pichani)
Mkaguzi Msaidizi wa Jeshi la Polisi Dawati la Jinsia Mkoa wa Kinondoni, Inspekta Prisca Komba (kushoto) akiongozana na Ofisa Mkuu wa Idara ya Uhusiano na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania, Georgia Mtagahywa kuelekea ukumbini ambako aliongoza semina ya masuala ya jinsia iliyoandaliwa na kampuni hiyo kwa ajili ya wafanyakazi wake iliyofanyika Mlimani City jijini Dar es Salaam leo.

No comments: