Wednesday, December 24, 2014

MFUKO WA MAENDELEO YA JAMII CHACHU YA MAENDELEO WILAYA YA KOROGWE.

Kikosi kazi maalum kutoka Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo wakiongea na Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe Bw.Lucas Mweri walimpotembelea leo ofisini kwake kwa ajili ya kufuatilia na kufanya tathmini ya mikopo iliyokwishatolewa katika Halmashauri ya wilaya ya Korogwe.
Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe,Bw.Lucas Mweri akielezea changamoto mbalimbali wanazopata kutoka katika Mfuko wa maendeleo ya Vijana ikiwemo fedhaza mkopo kuwa ndogo, kwa kikosi kazi kutoka Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo walipomtembelea ofisini kwake leo kufuatilia na kufanya tathmini ya mikopo iliyokwishatolewa kutoka Mfuko wa Maendeleo ya Vijana.
Afisa Uchumi Mwandamizi kutoka Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo,Bw.Yohana Ngao akiongea na wajumbe wa kikundi cha HEKIMA walipowatembea leo katika kata ya Mazinde kujua changamoto gani wanakutana nazo tangu wapewe mikopo kutoka katika mfuko wa Maendeleo ya Vijana.
Afisa Maendeleo ya Jamii Bi.Sabitina Maneto akitoa maoni kwa Kikosi kazi kutoka Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo(hawapo Pichani),kuhusu jinsi ya kuboresha mfuko wa Maendeleo ya Vijana na Kuufanya uwe bora zaidi uku akikazia pesa kwenda moja kwa moja kwenye SACCOS baada ya kuja kwenye vikundi.
Wajumbe wa kikundi cha HEKIMA kutoka kata ya Muheza wakiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa kikosi kazi kutoka Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo walipowatembea leo ili kufanya ufuatiliaji na tathmini ya mikopo iliyokwishatolewa kwa kikundi hicho.
Mjumbe wa kikundi cha HEKIMA kata ya Mazinde Rashid Salum(mwenye shati la bluu),akiwaonyesha Mradi wa Matofali uliotokana na pesa za Mfuko wa Maendeleo ya Vijana,Bw.Yohana Ngao ambae ni Afisa Uchumi Mwandamizi kutoka Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo(katikati) na Afisa Maendeleo ya Vijana Halmashauri ya Wizara ya Korogwe Bw.Mhinzi.
Wajumbe wa Kikosi kazi kutoka Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo wakiskiliza kwa makini maelezo kutoka kwa Katibu wa kikundi kisicho cha kiserikali-MOIDES(hayupo pichani),Bw.Nurdin Imam jinsi walivyotumia pesa walizopewa kutoka Mfuko wa Maendeleo ya Vijana.
Afisa Uchumi Mwandamizi kutoka Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo,Bw.Yohana Ngao(wa kwanza kulia) akiskiliza maoni kutoka kikundi cha Nyota Alfajiri ambao wameanzisha mradi wa kutengeneza Matofali na kuuza Asali ambapo walichukua mkopo wa shilingi milioni mbili na kurudisha kiasi cha shilingi laki 732,000 wakiwa wamefata taratibu zote za kurudisha mkopo ndani ya mwezi mmoja.
Wajumbe wa Kikosi kazi kutoka Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo wakiaangalia moja ya mradi wa matofali kutoka kikundi cha Nyota Alfajiri uliofanikiwa kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Vijana.Kikundi hicho kimetengeneza matofali elfu kumi na nne(14,000) na wanajiandaa kuyauza ili kujiendeleza kimaisha.

No comments: