Wednesday, December 24, 2014

OLOLOSOKWAN WAJIWEKA TAYARI KUTIMIZA NDOTO YA KIJIJI CHA DIJITALI

DSC_0129
DSC_0192
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues akifafanua jambo nje ya maktaba inayofadhiliwa na UNESCO na kuwanufaisha wanafunzi wa shule ya sekondari Ololosokwani na vijana wa kata hiyo kupanua uelewa zaidi kwa kusoma vitabu mbalimbali wakati akikagua miradi mbalimbali inayofadhiliwa na shirika lake. Kushoto ni Diwani wa kata hiyo ambaye pia ni Mkurugenzi wa Irkiramat Foundation (RAMAT) Bw. Yannick Ndoinyo.
DSC_0356
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues akiwa kwenye mazungumzo na viongozi wa juu wa halmashauri ya kijiji wakati wa ziara yake kijijini hapo mwishoni mwa wiki iliyopita.
DSC_0422
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues katika picha ya pamoja na uongozi wa halmashauri ya kijiji cha Ololosokwan mara baada ya mazungumzo.
DSC_0427
Bi. Zulmira Rodrigues katika picha ya pamoja na baadhi ya wanakijiji wa kijiji cha Ololosokwan kata ya Ololosokwan wilayani Ngorongoro mkoani Arusha.
DSC_0432
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues katika picha ya pamoja na wakina mama wa kimasai wa kata ya Ololosokwan kijiji cha Ololosokwani wilayani Ngorongoro mkoani Arusha mara baada ya kikao na halmashauri ya kijiji hicho.
DSC_0440
Bi. Zulmira Rodrigues akiagana na baadhi ya wakinamama wa kimasai mara baada ya kikao cha halmashauri ya kijiji hicho.
DSC_0228
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues (kulia) akifafanua jambo wakati wa kukagua eneo ambalo mitambo na miundombinu ya mradi itawekwa kwenye sehemu iliyotengwa na halmashauri ya kijiji kwa ajili ya kijiji cha dijitali cha Samsung. Kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa bodi ya RAMAT, Pokare Koitumet, Diwani wa kata hiyo ambaye pia ni Mkurugenzi wa Irkiramat Foundation (RAMAT) Bw. Yannick Ndoinyo pamoja na Chifu wa kijiji cha Ololosokwan kata ya Ololosokwan wilayani Ngorongoro mkoa wa Arusha.
DSC_0204
Muonekano wa eneo hilo huku Bi. Zulmira Rodrigues akiendelea kulikagua.

No comments: