Friday, May 6, 2016

MKUU WA MKOA WA MBEYA AZINDUWA RASMI MASHINDANO YA UMISETA LEO JIJINI MBEYA YANAYODHAMINIWA NA COCACOLA..

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mh.Amos Makalla akisalimiana na baadhi ya Wachezaji wa Timu za Shule za Sekondari zilizo shiliki katika Uzinduzi huo wa Mashindano ya Umiseta kwa Shule za Sekondari Mkoa wa Mbeya, ambapo Shule zote zilizo Shiriki katika Mashindano hayo Yanayotarajia kuanza hivi Karibuni katika Viwanja Mbalimbali Mkoani hapo walipewa Zawadi ya Vifaa vya Michezo kwa kila Shule iliyo Shiriki Sambamba na Vinywaji kutoka katika Kampuni ya Kuzalisha Vinywaji vya Soda Cocacola Ambao ndio Wadhamini Wakuu wa Mashindano hayo ya Umiseta Mwaka huu.
Kikundi cha Waburudishaji Jijini Mbeya kikitoa Burudani katika Uzinduzi huo wa Mashindano ya Umiseta Mwaka 2016 ulio fanyika katika Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya.
Baadhi ya Wanamichezo kutoka Shule za Sekondari Jijini Mbeya wakionyesha Umahiri wao katika Michezo...
Mmoja kati ya Wanafunzi akipewa Huduma ya Kwanza kutoka kwa Wanafunzi wenzake Mara baada ya kupoteza Fahamu kwa kukosa Hewa katika Hafra hiyo iliyofanyika katika Uwanja wa Kumbukumbu Sokoine Jijini Mbeya.
Baadhi ya Wanafunzi waliohudhuria Hafra hiyo ya Uzinduzi wa Mashindano ya Umiseta uliofanyika katika Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya.
PICHA ZOTE NA MR.PENGO MMG MBEYA.





No comments: