Thursday, February 18, 2016

Ziara ya Naibu Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano.

 Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Eng.Edwin Ngonyani (katikati) akielekezwa jambo na Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Bw.Magid Hemed alipofanya ziara yake ya kutembelea Wilaya hiyo kwa kuangalia mradi wa ujenzi wa daraja la Ruvu chini na bandari ya Bagamoyo.
 Naibu Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Eng.Edwin Ngonyani (katikati) akionyeshwa ramani itakapojengwa bandari ya Bagamoyo kutoka kwa Msimamizi wa Mradi wa Upanuzi wa Bandari hiyo kutoka Mamlaka ya Bandari nchini Bw. Alexender Ndibalema (Kushoto) katika ziara yake ya kutembelea Wilaya ya Bagamoyo.
  Eneo ya Chuo cha Uvuvi cha Mbegani Wilayani Bagamoyo ambayo ipo katika mpango wa kubadilishwa na kuwa Bandari ya Bagamoyo.
 Naibu Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Eng.Edwin Ngonyani (kulia) akisalimiana na Mafundi wa kampuni ya Ujenzi ya ESTIM inayojenga daraja la Ruvu chini katika barabara ya Bagamoyo kwenda Msata katika ziara yake ya kutembelea Wilaya ya Bagamoyo.
 Naibu Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Eng.Edwin Ngonyani (kulia) akielekeza jambo wakati alipotembelea ujenzi wa daraja la Ruvu chini katika barabara ya Bagamoyo kwenda Msata , wanaongalia ni Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Mhe. Magid Hemed (katikati) na Kushoto ni Mbunge wa Bagamoyo Mhe. Shukuru kawambwa.
  Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Eng.Edwin Ngonyani (kushoto) akimsikiliza Mhandisi wa mradi wa ujenzi wa daraja la Ruvu chini Bw. Adam Makiba(Kulia) wakati wa ziara ya kutembelea Wilaya ya bagamoyo pamoja na miradi ya ujenzi wa Bandari na daraja .
 Ujenzi wa daraja la Ruvu chini unavyoonekana katika picha ambapo unatarajiwa kumalizika mwishoni mwa mwaka huu.
  Naibu Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Eng.Edwin Ngonyani (kushoto) akipata maelezo kuhusu ukarabati wa barabara ya Msata kutoka kwa Mhandisi wa mradi wa ujenzi huo Bw. Adam Makiba wakati wa ziara ya kutembelea Wilaya ya bagamoyo pamoja na miradi ya ujenzi wa Bandari na daraja la Ruvu chini.
Barabara ya Bagamoyo kwenda Msata inavyoonekana katika picha baada ya kubainika mapungufu yake hata hivyo Mkandarasi ameahidi kufanyia kazi mapungufu hayo.
(Picha na Lorietha Laurence-Maelezo)

No comments: