Sunday, October 25, 2015

WAKAZI WA JIJI LA MBEYA WAJITOKEZA KWA WINGI KUPIGA KURA, MADUKA YAFUNGWA KUAJILI YA UCHAGUZI.....

Wakazi wa Jiji la Mbeya Mjini wajitokeza kwa wingi kupiga kura katika Vituo mbalimbali walivyo jiandikishia kuajili ya kupiga Kura kama waonekanavyo hapo katika Picha ni baadhi ya watu wakiwa katika kituo kilichopo Mtaa wa Mkombozi Jijini Mbeya wakiwa wamepanga Foleni kuajili ya kupiga Kura.
Baadhi ya Wapiga kura wakiwa katika Foleni..

Hapa ni eneo la Mwanjelwa maharufu kwa Jina la Mtaa wa kongo likiwa Pweke kuajili ya uchaguzi hakuna alie leta Biashara yake hapa siku hii ya leo..

Baadhii ya Maduka ya Vitu vya Jumla na Lejaleja yakiwa yamefungwa Eneo la Kabwa Stendi..

Jeshi la Polisi linaendelea kuzungukia Mitaa mbalimbali kuhakikisha hali ya Usalama  jijini mbeya Inakuwa shwari katika kipindi hiki cha uchaguzi.


 Hali ni shwari kwa jiji lote la Mbeya.

No comments: