Saturday, October 17, 2015

STIVE RNB, BERDON MNYAMA, DAVY VAN STAR NA PETRONIA WALIVYO SHAMBULIA JUKWAA KATIKA UZINDUZI WA WIMBO WA BERDON - NASIKIA HAMU.

Mwanamuziki Machachari anaekosha wengi kwa uimbaji wake wa Muziki wa kizazi Kipya ufahamikao kwa Jina la (RnB) Steve wa Rnb akitumbuiza katika Shoo ya Uzinduzi wa Wimbo wakwake Berdon Mnyama uendao kwa Jina la "Nasikia Hamu" Uzinduzi uliofanyika katika Ukumbi wa Hopeville Soweto jijini Mbeya.
Mwanamuziki wa Muziki wa kizazi kipya Berdon Mnyama akifanya yake katika Uzinduzi wa Wimbo wake Mpya uendao kwa Jina la "Nasikia Hamu" Uzinduzi uliofanyika katika ukumbi wa Hopeville Soweto jijini Mbeya.
Mwana Harakati Davy Van Star akitusua katika Shoo hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa Hopeville Soweto jijini Mbeya.
Baadhi ya Wanamitindo wanaofanya vizuri kabisa katika masuala ya Mitindo wakiwa Meza moja wakiongozwa na Mwanadada Petronia wapili kulia katika uzinduzi wa Wimbo wakwake Berdon Mnyama uendao kwa Jina la "Nasikia Hamu" Uzinduzi uliofanyika katika ukumbi wa Hopeville Soweto jijini Mbeya.
ILIFANA SANA.

No comments: