Monday, July 13, 2015

Timu ya Jimbo la Mkunazini Yaingia Nusu Fainali Kombe la Bonaza la Masauni Cup...

Kamanda wa Vijana akikagua timu ya Muembeladu wakati wa mchezo wa mwisho wa Bonaza la Masauni Cup.linalofanyika uwanja wa malindi Zanzibar, Mchezo huo umeshindwa kumalizika kutokana na Viongozi wa timu ya Muembeladu kuitoa timu yao kwa madai ya mchezaji wa timu ya Mkunazini kudaiwa kumpiga mpenzi wa timu hiyo.
Kamanda wa Vijana akikagua timu ya Mkunazini wakati wa mchezo wa mwisho wa Bonaza la Masauni Cup.linalofanyika uwanja wa malindi Zanzibar, Mchezo huo umeshindwa kumalizika kutokana na Viongozi wa timu ya Muembeladu kuitoa timu yao kwa madai ya mchezaji wa timu ya Mkunazini kudaiwa kumpiga mpenzi wa timu hiyo.
Kikosi cha timu ya Muembeladu kilicho shindwa kumaliza mchezo wao wa mwisho na timu ya Mkunazini timu hii ilihitaji ushindi wa mabao 3--0 ili kuweza kusonga mbele ya Bonaza hilo kuingia nusu fainali, mchezo huo umemalizi kabla ya wakati wake zikiwa zimebaki dakika 4 mchezo kumalizika. 
Kikosi cha timu ya Mkunazini kinachotinga Nusu Fainali leo usiku katika viwanja vya Mnazi mmoja na Timu ya Kikwajuni Juu.
Kocha wa timu ya Muembeladu akitowa maelezo kwa wachezaji wa timu yao kabla ya kuaza kwa mchezo wa Bonaza Masauni Cup. 
Wachezaji wa Timu ya Mkunazin wakiwania mpira wakati wa mchezo huo wa mwisho kukamilisha mzunguko wa kwanza. 
         Kipa wa timu ya Mkunazini akiokoa mpira wakati wa mchezo wao na timu ya Muembeladu
           Mchezaji wa timu ya Mkunazini akimpita mchezaji wa timu ya Muembeladu.
Mchezaji wa timu ya Muembeladu akiwa na mpira baada ya kumpita mchezaji wa timu ya Mkunazini akiwa chini.
Kiongozi wa Timu ya Mkunazini akitowa maelezo kwa wachezaji wake wakati wa mapumziko ya kipindi cha kwanza timu hizo zikiwa sare bila ya kufungana.
                        Golikipa wa timu ya Mkunazini akitowa maelezo kwa wachezaji wake.
Kocha Timu ya Muembeladu akitowa maelezo ya ushindi kwa wachezaji wake wakati wa mapumziko,Timu ya Muembeladu ilihitaji kushinda 3--0 ili kuweza kuingia nusu fainali yo Bonaza hilo. 
Mchezaji wa timu ya Mkunazini akiokoa mpira golini kwake huku mchezaji wa timu ya Muembeladu akiwa karibu
Mchezaji wa timu ya Mkunazini akimpita mchezaji wa timu ya Muembeladu wakati wa mchezo wao wa mwisho wa Bonaza Masauni Cup.Timu hizo zimetoka sare, baada ya mchezo huo kuvunjika kutokana na fujo za wapenzi wa timu hiyo  
Mchezaji wa timu ya Mkunazini anayedaiwa kampiga gunu mpenzi wa timu ya Muembeladu wakati akiokoa mpira na kuagukia katika eneo la timu hiyo na kutokea fujo hiyo iliosababisha mchezo huo kuvunjika zikiwa zimebaki dakika nne za mchezo huo.
Kiongozi wa Timu ya Mkunazini na Mchezaji wa Zamani wa timu ya Taifa Amour Azizi akimsihi kocha wa timu ya Muembeladu kuendelea na mchezo huo baada ya kuchukua uamuzi wa kuitoa timu yake nje

No comments: