Wednesday, June 3, 2015

MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO LEONIDAS GAMA AKABIDHIWA MRADI WA UJENZI WA UKUMBI WA CHAKULA ULIOFADHILIWA NA TANAPA.

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ,Leonidas Gama akisalimiana na viongozi wa wilaya ya Rombo mara baada ya kuwasili katika shule ya sekondari Olele iliyopo kata ya Olele kwa ajili ya kukabidhi Mradi wa ujenzi wa ukumbi wa Chakula uliojengwa kwa ufadhili wa Shirika la Hifadhi za Taifa , Tanzania (TANAPA).
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama pamoja na mkuu wa wilaya ya Rombo Lembris Kipuyo wakifurahia nyimbo iliyokuwa ikiimbwa na wanafunzi wa shule ya  sekondari ya Olele wakati alipofika kwa ajili ya uzinduizi na makabidhiano rasmi ya ukumbi wa chakula uliojengwa kwa ufadhili wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA).
RC ,Gamana iongozi wengine wakiskiliza nyimbo iliyokuwa ikiimbwa na kwaya ya shule ya sekondari Olele wilayani Rombo.
Kutokana na hali ya mvua iliyokuwepo wakati wa makabidhiano ya ukumbi wa chakula,mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro ,Leonidas Gama alilazimika kubadili meza kuu na wao wakaa eneo ambalo pia lilikuwa na mvua huku akisema ni vyema mvua ikawanyeshea wote pamoja na wananchi.
Jengo la Ukumbi wa Chakula lililojengwa kwa ufadhili wa Shirika la  Hifadhi za Taifa (TANAPA) katika shule ya sekondari Olele wilayani Rombo.
Meneja Ujirani Mwema kutoka Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Ahmed Mbugi akitoa taarifa kuhusiana na ujenzi wa ukumbi wa Chakula katika shule ya sekondari Olele.
Baadhi ya wananchi katika kata ya Olele. 
Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania,TANAPA,Ibrahim Musa akizungumza wakati wa hafla fupi ya kukabidhi mradi wa ujirani mwema wa ujenzi wa ukumbi wa Chakula katika shule ya sekondari Olele wilayani Rombo.
RC,Gama na DC,Kipuyo wakilowa kutokana na mvua iliyokuwa ikiendelea kunyesha.
Wanafunzi katika shule ya sekondari Olele wakifuatilia hotuba ya viongozi waliofika shuleni hapo kwa ajili ya makabidhiano ya ukumbi wa chakula uliojengwa na TANAPA.
Mkuu wa wilaya ya Rombo ,Lembris Kipuyo akizungumza katika hafla hiyo.
Wakazi wa kata ya Olele.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama akihutubia wananchi waliofika katika hafla fupi ya makabidhiano ya ukumbi wa chakula uliojengwa katika shule ya sekondari Olele wilayani Rombo kwa ufadhili wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA)
Mkuu wa mkoa wa Kilimajaro ,Leonidas Gama akikagua jengo hilo.
Na Dixon Busagaga wa Globu aya Jamii Kanda ya Kaskazini.

No comments: