Thursday, June 4, 2015

MATUKIO YA MAZISHI YA MHE. SAMWELI NTAMBALA LWANGISA JANA JUMATANO JUNI 3, 2015 KITENDAGURO-BUKOBA.

Na Faustine Ruta, Bukoba
Mamia ya Waakazi wa Mji wa Bukoba na Vitongoji vyake wakiwemo na Wageni mbalimbali kutoka nje ya Mkoa huu na nje ya Nchi wamejitokeza kwa wingi kumzika marehemu Samuel Luangisa jana Jumatano juni 3, 2015 nyumbani kwake Kitendaguro nje kidogo na Mji wa Bukoba. Marehemu Samuel Luangisa ni miongoni mwa waasisi wa Taifa na katika vipindi tofauti alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Ziwa Magharibi(Kagera) Mbunge na Meya wa Manispaa ya Bukoba pamoja na nyadhifa nyingine.
Mbunge wa muleba kusini Prof Anna Kajumulo Tibaijuka
Wanakwaya Mbalimbali walihudhuria Mazishi hayo

Baadhi ya Viongozi wa dini(katikati) ni Askofu Msaidizi wa Jimbo la Bukoba, Methodius Kilaini
Taswira za picha enzi ya uhai wa Marehemu Mhe. Samuel LuangisaMerehemu Samwel Lwangisa alizaliwa mwaka 1932 na mauti yalimkuta New York Marekani tarehe 25.05.2015 na kuzikwa jana Jumatano juni 3, 2015 Nyumbani kwake Kitendaguro Bukoba.
Askofu Msaidizi wa Jimbo la Bukoba, Methodius Kilaini
Mwanae na Marehemu akitoa neno lake
Jeneza lililobeba Mwili wa Marehemu Mhe. Samuel Ntambala Luangisa
Kushoto ni Mkuu wa Mkoa Kagera Mkuu wa Mkoa wa Kagera John Mongella akiwa sambamba na Mbunge wa Bukoba Mjini kwa tiketi ya CCM, Khamis Sued Kagasheki katika Mazishi Mhe. Samwel Ntambala Lwangisa jana Nyumbani kwake KItendaguro Nje kidogo ya Mjini wa Bukoba. Picha na Faustine Ruta
Le Mutuz nae alikuwepo katika Mazishi hayo ya Mhe. Samweli Ntambala Lwangisa.
Kushoto ni Bw. Willy O. Ruta mkurugenzi wa kampuni mpya ya utalii Bukoba Tour akishuhudia Mazishi hayo.
Mzee aliyekuwa karibu na marehemu Lwangisa akitoa neno Taswira
kulia ni Bi. Rukia Kassim kiwa na Mama Mwainunu



Wengi pia walifuatilia kupitia kwenye Tv Screen zilizokuwa ukumbini kutokana na wingi wa Watu hivyo Tukio zima kuwafikia kupitia kwenye tv katika sehemu walipokuwa maeneo hayo vyema.
Sehemu ya Baadhi ya Wanaumoja
Mwili ukisitiliwa kaburini


Wageni Mbalimbali kutoka Nje ya Nchi walijumuika
Umati uliojitokeza katika mazishi.

bukobasports.com tunaipa pole Familia ya Marehemu Mh. Samweli Ntambala Lwangisa.
Basi kama tukiishi au kama tukifa, tu mali ya Bwana....Warumi 14:8

No comments: