Wednesday, April 15, 2015

AJALI YA BASI BWAWANI LIKIELEKEA MKOANI MBEYA,HAKUNA ALIYEPOTEZA MAISHA.

 Pichani ni basi aina ya Costa likitoka Dar es Salaam kuelekea Mbeya limepata ajali na kupinduka kama lionekavyo pichani juu baada ya kuyumba na kuacha njia eneo la Bwawani muda wa saa 12.30 jana jioni . Kuna majeruhi kadhaa ambao wanapatiwa matibabu katika kituo cha Afya cha Magereza ya Bwawani. Chanzo cha ajali kinasadikiwa kuwa ni mwendo kasi na utelezi kutokana na mvua iliyokuwa inanyesha wakati huo.

No comments: