Monday, March 23, 2015

WAWILI WAPOTEZA MAISHA KATIKA BASI LA MORNING STAR LILILOPATA AJALI JANA LIKITOKEA ITAMBOLEO KUELEKEA MBEYA.

                                       Basi hilo baada ya kupata ajali
                       Baadhi ya watu wakiwa wamefika kushuhudia ajali hiyo
Basi la morning star linalotoka ubaruku-mbeya likiwa limetumbukia katika mfereji baada ya kuacha njia kwa kile kilichoelezwa ni kusapuka tairi la mbele na kupoteza mwelekeo. Jana asubuhi. Watu wawili walifariki dunia akiwamo mtoto wa miezo 9 na mtu mzima mmoja na abiria wengine 23 walijerhiwa vibaya ambapo walipelekwa hospitali ya misheni ya chimala. Wengi wao walivunjika miguu,mikono na kujerhiwa vichwani.

Ajali hiyo ilitokea eneo la itamboleo nje kidogo na mji wa igurusi wakati likielekea Mbeya.

KWA HISANI YA MBEYA YETU BLOG.

No comments: