Monday, March 23, 2015

WATUMISHI WAPYA NISHATI NA MADINI WAASWA KUWA WABUNIFU NA WAADILIFU.

Mkurugenzi wa Utawala na Utumishi kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Mrimia Mchomvu (aliyesimama), akisisitiza jambo kwa Wafanyakazi wapya wa Wizara hiyo (hawapo pichani), wakati wa ufunguzi wa Mafunzo Elekezi uliofanyika Jumatatu - Machi 23, 2015, katika Ukumbi wa Elimu ya Watu Wazima – Dar es Salaam. Mkurugenzi Mchomvu alifungua rasmi mafunzo hayo kwa niaba ya Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara husika, Mhandisi Ngosi Mwihava.
Mkurugenzi wa Utawala na Utumishi kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Mrimia Mchomvu (aliyesimama), akisisitiza jambo kwa Washiriki wa Mafunzo Elekezi kutoka Wizara hiyo (hawapo pichani). Kushoto kwake ni Mkurugenzi Msaidizi – Sehemu ya Rasilimaliwatu, Lusius Mwenda akifuatiwa na Afisa Utumishi Mwandamizi, Joan Ndibalema. Mkurugenzi Mchomvu alifungua Mafunzo hayo Jumatatu – Machi 23, 2015 kwa niaba ya Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara husika, Mhandisi Ngosi Mwihava.
Washiriki wa Mafunzo Elekezi kutoka Wizara ya Nishati na Madini, wakiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa Utawala na Utumishi wa Wizara hiyo, Mrimia Mchomvu (Mstari wa mbele – Katikati). Kulia kwa Mkurugenzi ni Mkufunzi wa Mafunzo hayo kutoka Chuo cha Utumishi wa Umma akifuatiwa na Mkurugenzi Msaidizi – Sehemu ya Rasilimaliwatu kutoka Wizarani, Lusius Mwenda. Kushoto kwa Mkurugenzi Mchomvu ni Mkufunzi wa Mafunzo kutoka Chuo cha Utumishi wa Umma, Mariam Kuhenga. Wa kwanza – Kulia (mwenye Koti Nyeusi) ni Ofisa Utumishi Mwandamizi kutoka Wizarani, Joan Ndibalema.
Mmojawapo wa Washiriki wa Mafunzo Elekezi kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Ester Njiwa (aliyesimama), akitoa neno la shukrani kwa niaba ya Washiriki wenzake kwa Uongozi wa Wizara husika, kwa kuandaa mafunzo hayo. Mafunzo hayo ya siku tano (5), yalifunguliwa rasmi Jumatatu – Machi 23, 2015 na Mkurugenzi wa Utawala na Utumishi, Mrimia Mchomvu kwa niaba ya Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mhandisi Ngosi Mwihava.
Washiriki wa Mafunzo Elekezi kutoka Wizara ya Nishati na Madini, wakimsikiliza Mkurugenzi wa Utawala na Utumishi, Mrimia Mchomvu (aliyesimama), wakati wa ufunguzi wa Mafunzo hayo uliofanyika Jumatatu – Machi 23, 2015, katika Ukumbi wa Elimu ya Watu Wazima jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Msaidizi, Sehemu ya Rasilimaliwatu – Wizara ya Nishati na Madini, Lusius Mwenda (aliyesimama), akizungumza na Wafanyakazi wapya wa Wizara hiyo (hawapo pichani), wakati wa ufunguzi wa Mafunzo Elekezi Jumatatu Machi 23, 2015 katika Ukumbi wa Elimu ya Watu Wazima – Dar es Salaam.
Sehemu ya washiriki wa Mafunzo Elekezi kutoka Wizara ya Nishati na Madini, wakimsikiliza Mkurugenzi wa Utawala na Utumishi, Mrimia Mchomvu (hayupo pichani) wakati wa ufunguzi wa Mafunzo husika uliofanyika Jumatatu – Machi 23, 2015, katika Ukumbi wa Elimu ya Watu Wazima – Dar es Salaam. Mafunzo hayo yatahitimishwa Ijumaa – Machi 27, 2015.


Meza Kuu; Kutoka Kushoto ni Waratibu na Wakufunzi wa Mafunzo Elekezi kutoka Chuo cha Utumishi wa Umma, Mariam Kahanga na Dorah Nestory; Mkurugenzi wa Utawala na Utumishi kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Mrimia Mchomvu; Mkurugenzi Msaidizi – Sehemu ya Rasilimaliwatu kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Lusius Mwenda na Afisa Utumishi Mwandamizi kutoka Wizara hiyo, Joan Ndibalema. 

No comments: