Wednesday, March 25, 2015

MEYA MANISPAA KINONDONI ATEMBELEA MABONDENI, AWATAKA WATU KUHAMA KUOKOA MAISHA YAO.


Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuph Mwenda (mbele) akikagua mto Ng'ombe uliopo eneo la Mwananyamala Kisiwani, wakati wa ziara hiyo Nyuma yake ni Naibu Meya,Songoro Mnyonge.
Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuph Mwenda (wa pili kushoto) akimsikiliza Naibu Meya, Songoro Mnyonge wakati akimpa maelezo kuhusu mazingira ya Mto Kiboko uliopo katika Kata ya Tandale wakati wa ziara yake katika Manispaa hiyo, Dar es Salaam jana.
Mkazi wa Mtaa wa Bahi, Jomo Macha akimueleza Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuph Mwenda athari za mafuriko katika Mtaa huo, Kata ya Makumbusho wakati wa ziara ya Meya huyo jana. Wengine ni Watendaji wa Manispaa hiyo na wakazi wa eneo hilo.
Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuph Mwenda akitoa maelekezo kwa watendaji wa Manispaa hiyo kuhusu kutafuta ufumbuzi wa chemba ya majitaka iliyofurika katika Mtaa wa Balozi Msolomi wakati wa ziara yake. Kulia kwake ni Naibu Meya, Songoro Mnyonge na watendaji wa Manispaa hiyo.
Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuph Mwenda (kulia) akijadiliana jambo na Naibu Meya, Songoro Mnyonge wakati wa ziara aliyoifanya katika Mtaa wa Kimamba, Kata ya Makurumla kukagua athari za mafuriko na changamoto zake jana. Katikati ni Diwani wa Kata hiyo, Rajab Hassan.
Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuph Mwenda (kulia) akikagua athari za mafuriko katika moja ya nyumba za Mtaa wa Kimamba, Kata ya Makurumla alipofanya ziara yake katika Manispaa hiyo, Dar es Salaam jana. Kushoto ni Diwani wa Kata hiyo, Rajab Hassan.
Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Kimamba, Kata ya Makurumla, Mohamed shukuru akisisitiza jambo kwa Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuph Mwenda kuhusu mikakati wanayoifanya kuepuka mafuriko wakati wa ziara ya Meya huyo aliyoifanya katika Mtaa huo jana. Kushoto ni Naibu Meya, Songoro Mnyonge na Diwani wa Kata hiyo, Rajab Hassan.

No comments: