Friday, February 20, 2015

WAZIRI MKUU,MIZENGO PINDA ZIARANI KATIKA JIMBO LA ISIMANI NA KALENGA MKOANI IRINGA.

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na wauguzi wa Kituo cha Afya cha Mlowa katika jimbo la Ismani kabla ya kuzindua kituo hicho akiwa katika ziara ya mkoa wa Iringa Februari 19, 2015.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akipima mapigo ya moyo ikiwa ni ishara ya kuzindua kituo cha afya cha Mlowa katika jimbo la Isimani akiwa katika ziara ya mkoa wa Iringa Februari 19, 2015.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akimjulia hali mmoja wa wagonjwa waliolazwa kwenye kituo cha afya cha Mlowa katika jimbo la Isimani akiwa katika ziara ya mkoa wa Iringa Februari 19, 2015.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akikagua matrekta madogo maarufu kwa jina la Power Tiller yanayotumika katika shamba la kilimo cha umwagiliaji la Magozi katika jimbo la Ismani wakati alipolitembelea shamba hilo akiwa katika ziara ya mkoawa Iringa Februari 19, 2015. Watatu kulia ni Mkuu wa mkoa wa Iringa, Amina Masenza.

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na walimu na wanafunzi wa shule ya sekondari ya Kiwere katika jimbo la Kalenga wakati alipotembelea maabara ya Kemia na Fizikia ya shule hiyo akiwa katika ziara ya mkoa wa Iringa Februari 19, 2015.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akitazama mafunzo kwa vitendo ya kumfanyia upasuaji panya yaliyokuwa yakifanywa na wanafunzi wa kidato cha tatu, Rosemary Kapugi (kushoto) na Faudhia Ndunguru Wapili kushoto) wakati alipotembelea maabara ya Baiolojia ya shule ya sekondari ya Kiwere katika jimbo la Kalenga akiwa katika ziara ya mkoa wa Iringa, Februari 19, 2015.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizindua nyumba za walimu katika shule ya sekondari ya Kiwere katika jimbo la Kalenga akiwa katika ziara ya mkoa wa Iringa Februari 19, 2015. Kushoto ni Mkuu wa Shule hiyo, Blandina Nkondola na watatu kulia ni Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Gerlad Guninita.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizindua nyumba za walimu katika shule ya sekondari ya Kiwere katika jimbo la Kalenga akiwa katika ziara ya mkoa wa Iringa Februari 19, 2015. Kushoto ni Mkuu wa Shule hiyo, Blandina Nkondola na wapili kulia ni Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Gerlad Guninita.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza (kushoto) na Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Kiwere katika jimbo la Kalenga mkoani Iringa baada ya kuzindua nyumba za walimu shuleni hapo akiwa katika ziara ya mkoa wa Iringa Februari 19, 2015. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

No comments: