Tuesday, January 13, 2015

TANZANIA NA SAUDI ARABIA KUSHIRIKIANA KATIKA UHIFADHI WANYAMAPORI.

Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Lazaro Nyalandu (Mb) akisisitiza jambo katika mazungumzo na Mwana wa Mfalme wa Saudia Prince Bandar bin Saud bin Mohammad Al-Saud ambaye pia ni Rais wa Mamlaka ya Wanyamapori ya Saudi Arabia.
 Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Dk. Adelhem Meru (kati) akiongea katika mazungumzo baina ya ujumbe wa Tanzania na Saudi Arabia. Kulia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira Mhe. James Lembeli na kushoto ni Balozi wa Tanzania Saudi Arabia Prof. Abdillah Omari.
Mwana wa Mfalme wa Saudia Prince Bandar bin Saud bin Mohammad Al-Saud ambaye pia ni Rais wa Mamlaka ya Wanyamapori ya Saudi Arabia akiongea katika mazungumzo hayo.
Mkurugenzi Mkuu wa TANAPA Allan Kijazi akichangia jambo katika mazungumzo hayo. Wengine pichani kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori Herman Keraryo; Waziri Kivuli wa Maliasili na Utalii Mhe. Peter Msigwa; Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira Mhe. James Lembeli na Balozi wa Tanzania Saudi Arabia Prof. Abdillah Omari.
Ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Lazaro Nyalandu (wa tatu kushoto) ukiwa katika picha ya pamoja na Mwana wa Mfalme wa Saudia Prince Bandar (wa nne kushoto) jijini Riyadh, Saudi Arabia. Wengine kutoka kushoto ni Balozi wa Tanzania Saudi Arabia Prof. Abdillah Omari; Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Dk. Adelhem Meru; Waziri Kivuli wa Maliasili na Utalii Mhe. Peter Msigwa; Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira Mhe. James Lembeli; Mkurugenzi Mkuu wa TANAPA Allan Kijazi na Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori Herman Keraryo.
Ujumbe wa Mwana wa Mfalme wa Saudi Arabia ukifuatilia mazungumzo hayo.
Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Lazaro Nyalandu (kulia) akiwa na mazungumzo na (kutoka kulia) Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Dk. Adelhem Meru; Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira Mhe. James Lembeli na Waziri Kivuli wa Maliasili na Utalii Mhe. Peter Msigwa muda mfupi kabla ya kuanza kwa mazungumzo baina ya Tanzania na Saudi Arabia jijini Riyadh, Saudi Arabia.

No comments: