Maandamano
ya wanafunzi wa Shule ya Mtakatifu Catherine Laboure iliyopo kijiji cha
Masanga wilayani Tarime, mkoani Mara wakiwa na mabango yenye jumbe
mbalimbali za kukemea ukeketeji wakisindikiza dada zao wahitimu wa kituo
cha FGMT katika sherehe ya mahafali ya sita ya mabinti (Waiseke wa
kisasa) waliokwepeshwa msimu wa ukeketaji yaliyofanyika mwanzoni mwa
wiki.
Aidha
Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika
la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez
amewataka mabinti hao kuwa chachu ya mabadiliko katika jamii na kuwa
chanzo cha kubadili kizazi kijacho.
Alisema wamesimama madhubuti kupinga mila potofu na uonevu na kusema kwa kitendo chao wamewafanya wengine kuwaiga na kubadilika.
Alisema
ukeketaji ni mila potofu na kusema kwa msaada wa shirika la Umoja wa
mataifa la Mpango wa familia (UNFPA) na taasisi nyingine zinazopambana
na ukeketaji kwa kipindi cha miaka saba wamefanikiwa kuwoakoa wasichana
2001 wasikeketwe.
Aidha mabinti hao wameokolewa dhidi ya ndoa za utotoni, ujauzito wa mapema na kushindwa kuendelea na masomo.
Naye
Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya
watu duniani (UNFPA), Dkt Natalia Kanem amesema ni vyema mapambano dhidi
ya ukeketaji yakaendelea kwa kuwa wanaoshabikia ni viongozi wa kimila
na ngumu kuiondoa ila kwa juhudi za jamii yenyewe.
Katika
sherehe hizo ambapo pia askofu wa Musoma alikuwepo na viongozi wengine
wa kiserikali pia Ngariba walioacha kazi hiyo walikuwepo kuelezea ubaya
wa mila hiyo.
Suala la ukeketaji ni kitu cha kawaida katika mikoa ya Manyara 71%, Dodoma 64%, Arusha 57%, Singida 51% na Mara 40%.
Viongozi
waliopata muda wa kuzungumza walisema kwamba ukeketaji unatakiwa
kukomeshwa mara moja kwani ni tatizo si tu kwa jamii bali kwa wale ambao
wanafanyiwa kisaikolojia na kitabibu.
Wahitimu
mabinti 37 waliokwepeshwa msimu wa ukeketaji wa kituo cha TFGM cha
kijiji cha Masanga wakiwasili na maandamano kwenye sherehe za mahafali
ya sita ya kituo hicho.
Moja
ya kazi inayoifanywa na kituo cha Masanga ni ushauri wa kisaikolojia
kutokana na wasichana wengi kufika hapo wakiwa na matatizo makubwa ya
magonjwa na hasa msongo wa mawazo.
Katika
risala yao mabinti hao wameitaka serikali kufanyakazi yake kukabiliana
na ubabe unaofanywa na viongozi wa kimila wa kuwalazimisha kukeketwa
hata msimu unapokuwa umepita.
Mabinti
hao ambao wengi wametoka shule ya msingi na sekondari wameweza kuwekwa
hapo kwa msaada wa UNFPA ambao wametoa hela kupitia Children’s Dignity
Fund (CDF), .Wafadhili wengine ni Daughters of Charity of St. Vincent Du
Paul, na Askofu wa kanisa katoliki dayosisi ya Musoma, Michael
Msongazila
Mgeni
rasmi Waziri wa Kazi na Ajira Mh. Gaudentia Kabaka akisalimiana na
Mhashamu Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Musoma Mkoani Mara,
Michael Msongazila mara baada ya kuwasili kwenye mahafali hayo.
Kwaya
ya vijana ya mara ikiimba wimbo wa Taifa kabla ya kuanza kwa sherehe za
mahafali ya sita ya kituo cha kupambana na ukeketaji Masanga wilayani
Tarime mkoani Mara.
Mgeni
rasmi Mh. Kabaka, Bw. Alvaro Rodriguez na SSP. Simon Mrashani
wakishiriki kucheza wimbo maalum unaohamasisha kukataza vitendo vya uovu
vya Ukeketaji kwa watoto wa kike wakati wa mahafali hayo.
Meza kuu ikitoa heshima kwa wimbo wa taifa.
Mkurugenzi
wa Kituo cha kupambana na ukeketaji cha Masanga (TFGM), Tarime, mkoani
Mara, Sista Germaine Baibika akimkaribisha mgeni rasmi pamoja wageni
waalikwa kwenye sherehe ya mahafali ya sita ya mabinti waliokwepeshwa
msimu wa ukeketaji.
Mgeni
rasmi Waziri wa Kazi na Ajira Mh. Gaudentia Kabaka akifurahi jambo na
Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika
la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez kwenye
sherehe za mahafali hayo.
Mgeni
rasmi Waziri wa Kazi na Ajira Mh. Gaudentia Kabaka akizungumza kwenye
sherehe za mahafali ya sita ya mabinti waliokwepeshwa msimu wa
ukeketaji.
Mratibu
Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la
Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez akitoa
salamu za Umoja wa Mataifa katika sherehe za mahafali sita ya mabinti
waliokwepeshwa msimu wa ukeketaji.
Mkuu
wa Wilaya ya Tarime, mkoani Mara, Bw. John Henjewele akitoa salamu kwa
niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mara katika mahafali ya sita ya kituo cha
kupambana na ukeketaji cha kijiji cha Masanga (TFGM) cha wilayani
Tarime, mkoani Mara.
Mwakilishi
wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya watu duniani
(UNFPA), Dkt Natalia Kanem, akizungumza kwenye sherehe hizo.
Kaimu
kamanda wa polisi wa kanda maalum ya Tarime na Rorya SSP. Simon Mrashani
akieleza jinsi jeshi la polisi linavyoshiriki katika kupambana na
masuala ya unyanyasaji wa kijinsia likiwemo suala la kesi za ukeketaji
ambapo pia alitoa takwimu za kesi zilizoripotiwa kituoni mpaka sasa ni
141, huku 80 zikiwa Mahakamani na 20 zimetolewa hukumu.
Mtaalam
wa Mahusiano na Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania, Hoyce
Temu akifurahi jambo na baadhi ya wafanyakazi wenzake wakati wa sherehe
za mahafali hayo.
Wahitimu
37 wakila kiapo cha kutokubali kutoshiriki kukeketwa na kuwa mabalozi
wazuri kwenye jamii zao katika kuelemisha madhara ya ukeketaji kwa
wanaoendeleza mila na tamaduni hizo pindi warudipo majumbani. Kwa picha zaidi ingia humu
No comments:
Post a Comment