Sunday, January 4, 2015

REDIO YA JAMII MKOANI YAZINDULIWA KUSINI PEMBA.

DSC_0213
Meneja wa Redio Jamii Mkoani jimbo la Mkanyageni Mkoani Kusini Pemba, Bw. Ali Abbas akisoma risala ya kituo chake mbele ya mgeni rasmi Waziri wa Uwezeshaji, Ustawi wa Jamii, Vijana, Wanawake na Watoto visiwani Zanzibar, Mh. Zainabu Omari Mohammed (hayupo pichani) wakati wa sherehe za uzinduzi wa kituo hicho cha redio.
DSC_0183
Mabinti wa visiwani Pemba wakisoma utenzi wa kulishukuru shirika la UNESCO na ZBC kwa kuanzisha kituo hicho cha Redio jamii jimbo la Mkanyageni mkoani Kusini Pemba.
DSC_0239
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo visiwani Zanzibar, Juma Yakufi akisoma hotuba kwa niaba ya Waziri mwenye dhamani ya wizara hiyo wakati wa sherehe za uzinduzi wa Redio Jamii Mkoani jimbo la Mkanyageni mkoani Kusini Pemba uliofanyika mwishoni mwa wiki visiwani humo.
DSC_0252
Mkuu wa Wilaya ya Mkoani Kusini Pemba, Hemedi Selemani akitoa neno la shukrani wakazi wa mkoani jimbo la Mkanyageni pamoja na wageni waalikwa kwenye sherehe za uzinduzi wa Redio Jamii Mkoani ya Kusini Pemba uliofanyika mwishoni mwa wiki.
DSC_0276
Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez akizungumza kwenye uzinduzi wa Redio Jamii Mkoani ya Kusini Pemba uliofanyika mwishoni mwa wiki.
DSC_0315
Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez akimkabidhi cheti Meneja wa Redio Jamii Mkoani ya Kusini Pemba, Bw. Ali Abbas wakati wa sherehe za uzinduzi wa Redio jamii hiyo.
DSC_0186
Meza kuu.
DSC_0323
Mkuu wa Mkoa wa Mkoani jimbo la Mkanyageni Kusini Pemba, Bi. Mwanajuma Abdallah akizungumza machache na wakazi wa mkoani na kuwaasa kukitumia chombo hicho vyema katika kujiletea maendeleo na kupashana habari kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi kuzindua rasmi kituo hicho cha Redio Jamii.
DSC_0358
Waziri wa Uwezeshaji, Ustawi wa jamii, Vijana, wanawake na watoto, Mh. Zainab Omar Mohammed akisoma hotuba yake kwenye sherehe za uzinduzi wa kituo cha redio ya jamii jimbo la Mkanyageni, Mkoani Kusini Pemba.
DSC_0078
Pichani juu na chini ni baadhi ya wakazi wa Mkoani jimbo la Mkanyageni Kusini Pemba wakifuatilia kwa umakini hotuba ya mgeni rasmi kwenye sherehe za ufunguzi wa kituo hicho cha Redio Jamii.
DSC_0167
DSC_0378
Pichani juu na chini ni Waziri wa Uwezeshaji, Ustawi wa jamii, Vijana, wanawake na watoto, Mh. Zainab Omar Mohammed akikabidhi vyeti kwa baadhi ya wafanyakazi wa Redio Jamii Mkoani ya jimbo la Mkanyageni mkoani Kusini Pemba. Anayeshuhudia tukio hilo ni Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo visiwani Zanzibar, Juma Yakufi.
DSC_0388
DSC_0401
Mgeni rasmi Waziri wa Uwezeshaji, Ustawi wa jamii, Vijana, wanawake na watoto, Mh. Zainab Omar Mohammed akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa kituo cha Redio Jamii Mkoani iliyopo Kusini Pemba. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Mkuu wa Mkoa wa Mkoani jimbo la Mkanyageni Kusini Pemba, Bi. Mwanajuma Abdallah (mwenye mtandio wa bluu), Mkuu wa Wilaya ya Mkoani Kusini Pemba, Hemedi Selemani pamoja na Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez.
DSC_0403
Sasa kimezinduliwa rasmi....!
DSC_0465
Mgeni rasmi Waziri wa Uwezeshaji, Ustawi wa jamii, Vijana, wanawake na watoto, Mh. Zainab Omar Mohammed akitia saini kitabu cha wageni cha kituo cha Redio Jamii Mkoani Kusini Pemba kabla ya kukagua vifaa na studio ya kituo hicho.
DSC_0438
Mgeni rasmi Waziri wa Uwezeshaji, Ustawi wa jamii, Vijana, wanawake na watoto, Mh. Zainab Omar Mohammed akizungumza Live na wananchi wa jimbo la Mkanyageni mkoani Kusini Pemba mara baada ya kuzindua kituo cha Redio Jamii Mkoani ikiwa ni shamra shamra ya sherehe za Mapinduzi mwishoni mwa wiki kisiwani Pemba. Wanaoshuhudia ni Mkuu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na washika dau kutoka UNESCO.
DSC_0427
Mtangazaji wa kituo cha Redio Jamii Mkoani ya Kusini Pemba, Bw. Seif Mohammed akiwa kwenye mahojiano na Mgeni rasmi Waziri wa Uwezeshaji, Ustawi wa jamii, Vijana, wanawake na watoto, Mh. Zainab Omar Mohammed yaliyorushwa Live na kituo hicho mara baada ya kuzinduliwa.
DSC_0497
Mgeni rasmi Waziri wa Uwezeshaji, Ustawi wa jamii, Vijana, wanawake na watoto, Mh. Zainab Omar Mohammed katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Redio Jamii Mkoani, Wajumbe wa Bodi ya Redio Jamii Mkoani, wafadhili pamoja na baadhi ya wageni waalikwa.
Mgeni rasmi Waziri wa Uwezeshaji, Ustawi wa jamii, Vijana, wanawake na watoto, Mh. Zainab Omar Mohammed katika picha ya pamoja na wajumbe wa bodi ya Redio Jamii Mkoani jimbo la Mkanyageni Kusini Pemba.
DSC_0515
Mshauri na Mkufunzi kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Bi. Rose Haji Mwalimu akiwa kwenye picha na wanafunzi wake wa vituo vya redio jamii ya Mkoani na Micheweni mara baada ya sherehe za uzinduzi.
DSC_0158
Kikundi cha Ngoma ya Msembwe cha kisiwani Pemba kikitoa burudani kwenye uzinduzi wa Redio Jamii Mkoani uliofanyika mwishoni mwa juma Kusini Pemba.

No comments: