Sunday, January 25, 2015

Halmashauri ya Wilaya ya Chunya yachangia Shilingi Milioni 210 katika Mfuko wa Vijana na Wanawake kwa kipindi cha miaka miwili

Kaimu Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Chunya Bibi Ester Makalili akizungumza na ujumbe kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo walipomtembelea ofisini kwake kabla ya kukutana na vijana wa Wilaya hiyo kutoa mafunzo ya Ujasiriamali, Stadi za Maisha, Ujuzi na Mfuko wa Maendeleo ya Vijana jana katika Wilaya ya Chunya Mkoa wa Mbeya. Kushoto ni Mwenzeshaji kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi Ester Riwa na kushoto ni Mkuu wa Kituo cha Vijana Sasanda Mbeya Bw. Laurean Masele.
Mwezeshaji kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi Ester Riwa akitoa mada ya Ujuzi kwa vijana wakati wa semina ya Ujasiriamali, Stadi za Maisha, Ujuzi na Mfuko wa Maendeleo ya Vijana jana katika Wilaya ya Chunya Mkoa wa Mbeya.
Afisa Ushirika kutoka Wilaya ya Chunya Mkoa wa Mbeya Bw. Mwanyi Magambo akiwaelimisha vijana wa Wilaya ya Chunya umuhimu wa kuunda Saccoss ya Vijana itakayowawezesha vijana kuweka akiba na kukopeshana wakati wa semina ya Ujasiriamali, Stadi za Maisha, Ujuzi na Mfuko wa Maendeleo ya Vijana jana katika Wilaya ya Chunya Mkoa wa Mbeya.
Afisa Maendeleo ya Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Amina Sanga kushoto akizungumza na wanakikundi wa Ngozi group wanaosindika ngozi kwa njia ya asili na kutengeneza bidhaa za ngozi kwa kutumia ngozi walizosindika walipowatembelea kukagua mradi wao jana katika kijiji cha Mkwajini Wilaya ya Chunya Mkoa wa Mbeya. Wa pili kulia ni Mkuu wa Kituo cha Vijana Sasanda Mbeya Bw. Laurean Masele.
Kijana Meshaki Ngailo kushoto kutoka kikundi cha Vijana Bush Man Works kinachofanya kazi ya kuunga vyuma akizungumza na maafisa waliofika kukagua mradi wa kikundi chake wakati wa ziara ya kukagua miradi ya vijana wa Mkoa wa Mbeya.

No comments: