Miss
Tanzania Lilian Kamazima (kulia) akimkabidhi zawadi ya mwaka mpya
Msimamizi wa kituo cha kulelea watoto yatima cha New Life kilichopo
Boko, Mwanaisha Magambo kwa ajili ya watoto 102 waliopo kituoni hapo,
tukio hilo lilifanyika juzi.
Miss
Tanzania Lilian Kamazima (kulia) akiwa na Miss Kinondoni Maria Shila
wakiwa wamembeba mtoto aliekuwa kwenye kituo cha kulelea watoto yatima
cha New Life cha Boko, mtoto huyo alifikishwa hapo akiwa na siku nne tu
tangia kuzaliwa kwake.
Sehemu ya Watoto wanaolelewa katika kituo cha kulelea watoto yatima cha New Life kilichopo Boko,wakimsikiliza Miss Tanzania Lilian Kamazima.
Miss Tanzania Lilian Kamazima (kulia) akiwa na watoto katika kituo cha New Life cha Boko.
Redds
Miss Tanzania 2014 Lilian Deus Kamazima jumapili iliyopita alitoa
misaada ya vyakula vya aina mbalimbali kwa kituo cha New Life Orphans
Home kilichopo eneo la Boko nje kidogo ya jiji la D’salaam.
No comments:
Post a Comment