Mwezi
huu wa Disemba 2014,EFM redio ilianza kuwashukuru wasikilizaji wake kwa
kuanzisha “Kapu la sikukuu project”.
Madhumuni ya project hii ni kuwashukuru wasikilizaji wa redio ya 93.7
EFM kwa upendo walio uonyesha tangu kufunguliwa kwa redio hiyo mpaka
sasa.
Meneja
uhusiano ambae pia ni mmoja wa watangazaji wa kipindi cha Joto La
Asubuhi,Kanky Mwaigomole alisema kuwa makapu hayo ya sikukuu yalikua
yamejaa hasa vitu vya nyumbani.
“Tumehakikisha
ya kwamba kapu hili litakalo muendea mshindi na familia yake,iwe ni
furaha tosha kwani kapu mmoja limewekwa nyama,kuku,mafuta ya
kupikia,mchele,unga wa ngano na wa sembe,nyanya,vitunguu na kadhalika”,
alisema Mwaigomole.
Kanky Mwaigomole alisema kuwa utaratibu wa kushinda kapu hilo wala halikuwa na masharti magumu.
“Tulitumia
mziki mfupi bila maneno wa "merry christmas ya jingle bells" na
msikilizaji alitakiwa kusikiliza redio yetu mda wote,endapo pale
angesikia mwimbo huo wa jingle bells,anaandika ni mda gani umepigwa na
ni watangazaji gani waliupiga”,alisema.
Kanky
aliendelea kusema kwamba kwa yule ambae alipatia jibu ndio alipigiwa
simu siku ya leo na kuelekezwa kufwata kapu lake la sikukuu.
Washindi 30 walifanyikiwa kuitwa katika ofisi za EFM na kukabidhiwa makapu yao rasmi siku ya tarehe 24 mwezi wa Disemba 2014.
Mshindi wa kapu la sikukuu akipewa kapu lake na Mkuu wa
vipindi wa EFM Bwana Dickson Ponella (Dizo one)
Meneja Uhusiano wa EFM,Kanky Mwaigomole,akimsaidia mmoja wa washindi wa Kapu la sikukuu,kuingiza kwenye usafiri.
Mtangazaji wa kipindi cha gurudumu,Swebe,akimsaidia mmoja wa
washindi wa kapu la sikukukuu bwana Darisudi wa Bunju.
Bwana Mosheni Mosheni,akiwa na nduguye,walivyokuja kuchukua
kapu lao.
No comments:
Post a Comment