Thursday, May 26, 2016

KIJIPU UPELE KIGOGO MTO MSIMBAZI....

Katika Pita Pita za Libeneke lako la Globu ya Jamii Lilifanikiwa Kuzinasa Taswira Kutoka Katika Bonde la Msimbazi lililopo Kigogo Jijini Dar es salaam na kushuhudia Jinsi hali ilivyo kuwa ni Rafiki na Pendwa haswa kwa Wakazi wanao Lizunguka Eneo hilo.
Kwani Takataka zime Jaa katika Bonde hilo na Wakazi wa Eneo hilo hakuna lolote linalo fanyika ili kuweza kukabiliana na Changa Moto hiyo ya Kijipu Upele kilichopo katika mazingira yao  na badala yake baadhi yao wanaendelea kuongeza Takataka kwenye Eneo hilo.
Watoto waishio Katika Mazingira hayo ni Marafiki wakubwa wa Eneo hilo kwani hutumika Kama Njia pia ni kama Sehemu ya Michezo kama ambavyo Baadhi ya watoto waonekanao katika Taswira.
Watoto wa Mtaa huo wakiwa katika harakati za Kuokoteza Baadhi ya vitu Vinono Wanavyo Vipenda kama ambavyo walivyo Naswa na Kamera Yetu.

No comments: