Thursday, March 3, 2016

DK.KIGWANGALLA AFUNGUA RASMI JENGO LA WAGONJWA MAHUTUTI MUHIMBILI.

SERIKALI imesema kwa sasa itakuwa ikihudumia wagonjwa wote ndani ya nchi ikiwemo wale wagonjwa Mahututi ambao awali walikuwa wakipelekwa nje ya nchi. Hii ni baada ya kuendelea kuimarisha huduma hizo pamoja na kuwa na wataalam wa kutosha ambaio watapatiwa mafunzo zaidi.

Kauli hiyo imetolewa leo na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto, Mheshimiwa Dk. Hamisi Kigwangalla wakati wa kuzindua rasmi wodi ya Wagonjwa Mahututi (ICU) iliyopo katika jengo la Mwaisela katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, jijini Dar es Salaam.

Dk.Kigwangalla katika uzinduzi huo, amewapongeza watendaji wote waliofanikisha ikiwemo uongozi uliopita na ule wa sasa, Serikali pamoja na wadau wa sekta hiyo ya afya walioguswa na kuchangia upanuzi wa huduma za tiba ya wagonjwa hao Mahututi ambayo imewezeshwa kuwa na vifaa tiba vya kisasa huku ikiongezwa vitanda kutoka 8 hadi 25 kwa sasa.

Aidha, Dk. Kigwangalla ametoa shukrani ya kipekee kwa wadau waliojitolea kwa moyo wao kuchangia huduma hiyo ya wagonjwa Mahututi ikiwemo Shirika lisilo la Kiserikali la Gastrenterology Foundation kutoka Ujerumani na wadau wote kwa kuweza kufanikisha huduma hiyo kuweza kupatikana hapa nchini na kupunguza safari za nje ambazo zimekuwa zikiigharimu Nchi fedha nyingi.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Prof. Lawrence Museru (kushoto) akisoma hotuba maalum juu ya uzinduzi huo wa wadi ya wagonjwa Mahututi (ICU). Anayefuatia ni Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto, Mheshimiwa Dk. Hamisi Kigwangalla ambaye alikuwa mgeni rasmi. Wengine ni wadau waliowezesha kwa wodi hiyo akiwemo Rais wa shirika la Gastrenterology, Prf. Meinhard Classen (wa tatu kutoka kushoto) pamoja na Bingwa wa Magonjwa ya tumbo kutoka Misri, Prf. Abdel Meguid.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto, Mheshimiwa Dk. Hamisi Kigwangalla akifafanua jambo katika mkutano huoleo wakati alipokuwa mgeni rasmi mapema leo Machi 3.2016.
Dk.Kigwangalla akiwasili katika jengo la Mwaisela kwa ajili ya uzinduzi wa wodi ya wagonjwa Mahututi.
DK. Kigwangalla akisalimiana na mmoja wa wadau wa sekta ya afya wakati alipowasili katika jengo la Mwaisela
Dk Kigwangalla akijadili jambo na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Prf. Museru
Dk. Kigwangalla akisalimiana na mmoja wa wageni waalika katika tukio hilo
Prf.Maseru akijadiliana jambo na Rais wa shirika la Gastrenterology, Prf. Meinhard Classen (kushoto) na Dk. John wa JKCI.
Mlango huo wa kuingia ICU kabla ya uzinduzi rasmi.
Dk. Kigwangalla akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa wadi ya wagonjwa mahututi (ICU) katika jengo la Mwaisela. Wanaoshuhudia ni Rais wa shirika la Gastrenterology, Prf. Meinhard Classen (kulia) na Prf. Museru kushoto.
Dk. Kigwangalla pamoja na viongozi wengine wakiwa ndani ya ICU baada ya uzinduzi huo. Wengine ni Rais wa shirika la Gastrenterology, Prf. Meinhard Classen (kushoto) na kulia ni Prf. Museru ambaye ni Kaimu Mkurugenzi wa hospitali hiyo.
Dk. Kigwangalla akizungumza na wanahabari muda mfupi baada ya uzinduzi huo wa wadi ya wagonjwa mahututi katika jengo la Mwaisela. (Picha zote na Andrew Chale.)

No comments: