Saturday, February 27, 2016

VURUGU ZA MACHINGA ZAZUWA TAFRANI JIJINI MBEYA....

Baadhi ya Vibanda vya Biashara vya Wafanyabiashara Ndogondogo Maarufu kama Machinga Vikiteketea kwa Moto mara baada ya Wafanya Biashara hao wa Eneo la Sido na Stendi ya Kabwe Jijini Mbeya kuanzisha Vurugu Baada ya Kubomolewa Vibanda vyao vya Biashara katika maeneo waliyokuwa wakifanyia Biashara Zao.
Jitihada za kuzima Moto ulio washwa na Wamachinga wa Kabwe na Sido zikifanyika kutoka kwa Jeshi la Zima Moto Jiji la Mbeya katika Vurugu zilizo Dumu kwa Muda kuanzia Asubuhi ya Leo na kupelekea Wamachinga hao Kuchoma Matairi Barabarani na Baadhi ya Masalia ya Vibanda vyao mara baada ya Kubomolewa Vibanda vyao vya Biashara.
Jeshi la Polisi kikosi cha kutuliza Ghasia kikiwa Ngangari kuhakikisha hali ya Usalama ina kuwa Shwari na Vurugu kutoendelea...
Baadhi ya wapiga Debe wa Stendi ya Kabwe wakiwa hawana nongwa na Mtu bali wakiendelea kutimiza agizo la Rais Dkt.John Pombe Magufuli kufanya Usafi kila Juma Mosi ya mwisho wa Mwezi na hapo wakiwa Sambamba na Vifaa vyao vya kufanyia Usafi mbele ya Jeshi la Polisi kama waonekanavyo katika Taswira.
PICHA ZOTE NA MR.PENGO MMG MBEYA.

No comments: