Sunday, August 30, 2015

MSD YAZINDUA RASMI TAARIFA YAKE YA MWAKA 2013/2014 (ANNUAL REPORT).......


 Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa MSD, Profesa Idris Ali Mtulia (kushoto), akikata utepe kuashiria uzinduzi wa taarifa ya MSD ya mwaka 2013/2014 uliofanyika Ofisi za MSD Keko jijini Dar es Salaam jana. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa MSD, Cosmas Mwaifwani.
 Kaimu Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala wa MSD, Johnson Mwakalitolo, akizungumza katika uzinduzi huo.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya MSD, Profesa Idris Ali Mtulia, akizungumza katika uzinduzi huo.
 Mkurugenzi wa Tehama  wa MSD, Issaya Mzolo, akizungumza katika hafla ya uzinduzi huo.
Ofisa Uhusiano Mkuu wa MSD, Etty Kusiluka (kushoto), akizingumza kwenye uzinduzi huo. Kulia ni Meneja wa Uhasibu wa MSD, Sako Mwakalobo.
Keki ya Birthday ya Kaimu Mkurugenzi wa MSD, Cosmas Mwaifwani katika muonekano.
Kaimu Mkurugenzi wa MSD, Cosmas Mwaifwani (kushoto), akikata keki hiyo aliyoandaliwa na wafanyakazi wenzake wakati wakimpongeza kutimiza miaka 55 ya kuzaliwa kwake. Kulia ni Katibu Muhtasi wa Mkurugenzi wa MSD, Doreen Josia. Wafanyakazi hao waliamua kumpongeza Mwaifwani baada ya kumalizika kwa uzinduzi wa ripoti hiyo.
Mwaifwani akimlisha keki, Mkurugenzi wa Shughuli za Kanda na Huduma kwa Wateja wa MSD, Edward Terry.
Hapa ni zamu ya Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya MSD, Profesa Idris Ali Mtulia akilishwa keki.
Mkurugenzi wa Shughuli za Kanda na Huduma kwa Wateja wa MSD, Edward Terry, akimlisha keki, Kaimu Mkurugenzi wa MSD, Cosmas Mwaifwani.
Hapa Katibu Muhtasi wa Mkurugenzi MSD, Dinah Dileya (kushoto), akilshwa keki.
Ofisa Uhusiano wa MSD, Benjamin Massangya (kulia), akigawa ripoti hiyo kwa wafanyakazi wa MSD.
Ofisa Uhusiano Mkuu wa MSD, Etty Kusiluka (kushoto), akizingumza kwenye uzinduzi huo.
Wafanyakazi wa MSD, wakifuatilia uzinduzi huo.
Wafanyakazi wa MSD, wakiwa kwenye uzinduzi huo.
Ni furaha tupu katika uzinduzi huo na hafla ya wafanyakazi hao kumpongeza Kaimu Mkurugenzi wa MSD, Cosmas Mwaifwani kutimiza miaka 55 tangu azaliwe.
Viongozi wa MSD wakiwa kwenye uzinduzi huo.
Hii ni timu ya wajumbe walioandaa ripoti hiyo ya mwaka 2013/2014. 'Big Up wajumbe kwa kazi nzuri.

Na Dotto Mwaibale
BOHARI ya Dawa (MSD) imezindua rasmi taarifa yake ya mwaka 2013/2014 (Annual Report), ambayo ilizinduliwa Dar es Salaam jana na Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa MSD, Profesa Idris Ali Mtulia.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa taarifa hiyo, Profesa Mtulia alisema kupanda kwa huduma za usambazaji dawa, upatikanaji wa dawa kutoka asilimia 55 hadi 85 ni jambo la kujivunia.

Kaimu Mkurugenzi wa MSD, Cosmas Mwaifwani alisema mpango wa MSD kwa sasa ni kuanzisha maduka ya dawa ambayo yataendeshwa na MSD ambapo kwa kuanzia hivi karibuni litazinduliwa mkoani Mbeya na baadae itafuatia mikoa Kanda za  Dar es Salaam, Mwanza na Moshi.

No comments: