Wednesday, July 1, 2015

SIMBA SPORT CLUB YAANDIKA HISTORIA,WAZINDUA KADI MPYA...

Afisa MtendajiMkuuwa EAG Group Imani Kajula  Rais wa Simba Sport Club Evans Aveva Pamoja na Makamu wa Rais wa Club ya Simba Geofrey Nyange ‘Kaburu Wakiwa wameshika Mfano wa Kadi ya Club Hiyo waliyoizindua.
Klabu ya Simba leo hii imeandika historia kwa kuzindua Kadi Mpya za Wanachama ambazo zinamwezesha  kila Mwanachama wa  Simba  kupata  bima  ya maisha  hadi  Tsh 250,000 ikiwa atafiwa  na  mwenza au mtoto au yeye  mwenyewe  kupitia  bima  ya  maisha   iitwayo Simba Pamoja. Pia Simba  imezindua  Kadi za watoto yaani Simba Cubs. 
Rais wa Simba Sport Club Evans Aveva Akimkabidhi Mtoto  Iqram Ally Kadi ya Simba Cubs waliyoizindua leo wanaoshuhudia ni Afisa Mtendaji Mkuu wa EAG Group Imani Kajula (kulia) Pamoja na Makamu wa Rais wa Club ya Simba Geofrey Nyange

Akizungumza wakati wa uzinduzi Rais wa Simba Evans Aveva alisema ‘’Simba inaendeleza falsafa yetu ya utendajii  kifanya kazi ‘’maneno machache vitendo vingi’’, baada ya kuboresha upatikanaji wa taarifa kupitia mtandao kwa kuzindua tovuti yenye taarifa na huduma mbalimbali ndani yake, leo tumewaita  hapa  kuandika historia mpya kwa wana Simba na hususani wale wanaota ka kuwa wanachama wa Simba’’.
Aliongeza  kusema ‘’ Simba inapenda kuwajulisha kuwa sasa mpenzi wa Simba anayetaka kuwa mwanachama anaweza kuomba kupata kadi ya wanachama kupitia tovuti ya Simba yaani www.Simbasports.co.tz . Napenda mtambue hii ni historia katika  ukanda huu kuweza kutumia  teknojia kufikia wanachama, Sisi  ni wakisa  sana  tunaona  mbele!.
AfisaMtendajiMkuuwa EAG Group Imani Kajula (Kulia) Akielezea Jambo  Akiwa Ameambatana na Rais wa Simba Sport Club Evans Aveva (katikati) Wakati wa Uzinduzi wa Kadi Hiyo ya Simba Sport  Club Pamoja na Makamu wa Rais wa Club ya Simba Geofrey Nyange ‘Kaburu
Kwa  upande wake Afisa Mtendaji  Mkuu  wa EAG Group ambao ni washauri watekelezaji wa mikakati  ya masoko na  biashara Imani  Kajula  alisema
‘’ Uanzishwaji  wa  Kadi  ya  Simba Cubs itawawezesha watoto sio tukutambuliwa  kuwamemba  wa  Simba, bali  pia  kupata  punguzo   kubwa au kuingia  bure  kwenye  matukio  yanayo  andaliwa  na  Simba Sports Club. Pia  maduka  mbalimbali  yatatoa  punguzo  kwa  watoto  wenye  Simba Cub Card.
Wote  mna  jua fika  kuwa  mapenzi   hujengwa, Simb  aina lenga kujenga msingi  imara  wa kuendeleza  wanachama  na  wapenzi wake’’.

No comments: