Wednesday, July 1, 2015

MBUNGE MBATIA AJIANDIKISHA KATIKA DAFTARI LA WAPIGA KURA KIJIJINI KWAO KWAMARE JIMBONI VUNJO...

Mbunge wa kuteuliwa,Mh James Mbatia akiwasili katika kijiji cha Kirua Vunjo Magharibi na kupokelewa na msaidizi wake Hamis Hamis kwa ajili ya zoezi la kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura kupitia BVR.
Mbunge wa kuteuliwa ,Mh James Mbatia akisalimiana na wananchi mara baada ya kuwasil katika kijiji cha Kwamare kata ya Kirua Vunjo Magharibi Jimbo la Vunjo kwa ajili ya kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura.
Mbunge James Mbatia akitoa maelezo yake kwa mmoja wa maofisa wa zoezi la uandikishaji katika daftari la kudumu la wapiga kura kupita mfumo wa BVR.
Mbunge James Mbatia akichukuliwa alama za vidole wakati wa zoezi la uandikishaji katika kijiji cha Kwamare kata ya Kirua Vunjo.
Mh Mbatia akitia saini katika kifaa kimoja wapo kwa ajili ya kuweka kumbukumbu.
Mh Mbatia akiweka vidole gumba kwa ajili ya kuchukuliwa alama.
Afisa uandikisha akimkabidhi Mh Mbatia kitambulisho chake mara baada ya kumaliza zoezi la uandikishaji.
Mh Mbatia akionesha kitambulisho maalumu kwa ajili ya zoezi la kupiga kura litakalofanyika hapo baadae mwezi oktoba.
Msaidizi wa Mh Mbatia ,Hamis Hamis akikabidhiwa kitamburisho chake mara baada ya kumaliza zoezi la kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura.
Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

No comments: