Tuesday, June 23, 2015

KATIBU MKUU WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI ATEMBELEA BANDA LA WIZARA YAKE KATIKA MAONYESHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA KATIKA VIWANJA VYA MNAZI MMOJA

Afisa wa Jeshi la Magereza nchini, Nsajigwa Mwankenja akitoa maelezo kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil kuhusu shughuli zinazofanywa na Jeshi hilo, wakati Katibu Mkuu alipotembelea Banda la Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, wakati wa maonyesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil, akipata maelezo kutoka kwa Maafisa wa Uhamiaji kuhusu shughuli zinazofanywa na Idara hiyo, wakati alipotembelea banda la Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi katika Maonyesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil akisoma vipeperushi vya Idara ya Uhamiaji wakati alipotembelea banda la Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi katika maonyesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika viwanja vya Mnazi mmoja jijini Dar es Salaam.
Afisa wa Jeshi la Magereza (kulia) akimuonyesha Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil, aina ya mbegu bora ya muhugo inayolimwa na Jeshi hilo katika mashamba yake, wakati alipotembelea banda ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi katika Maonyesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil akisaini kitabu cha wageni wakati alipotembelea banda la Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa katika maonyesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Bima Tanzania (TIRA), Israel Kamuzora akipata maelezo kutoka kwa Afisa Habari Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa, Rose Mdami, ya jinsi ya kujaza fomu ya kuomba Kitambulisho cha Taifa, wakati Mkurugenzi Kamuzora alipotembelea banda la Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) katika maonyesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.

No comments: