Monday, May 11, 2015

WAZIRI MKUU PINDA AFUNGUA MAONYESHO YA ELIMU MKOANI DODOMA

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akimkabidhi Sista  Flosy Sequeire, Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Saint Francis ya Mbeya tuzo maalum ya kutambua  ufalu mzuri wa wanafunzi wa shule  hiyo  wakati alipofungua  maadhimisho ya wiki ya Elimu kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma Mei 11, 2015. Wemgne kutoka kushoto ni  Waziri wa Elimu na Mafunzi ya Ufundi, Dkt. Shukuru Kawambwa, Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Seriklai za Mitaa, Kassim Majaliwa, Mkuu wa mkoa wa Dodoma, Chiku Galawa na Mbunge wa Viti Maalum, Margareth Sitta.
 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana naWaziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri  Mkuu, Jenista Mhagama baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Dodoma  Mei 11, 2015  kwa ajili ya kikao cha Bunge kinachotarajiwa kuanza Mei 12, 2015.  Katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Chiku Galawa.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akimkabidhi pikipiki Mratibu wa Elimu wa Kata ya Ibiwhwa wilayani Bahi, Jacob Mwakalambo ikiwa ni chombo cha kumwezesha kutekeleza majukumu yake katika maadhimisho ya wki ya elimu wenye uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma leo, Kulia ni Naibu waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Kassim Majaliwa.
 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na mzee wa Kihadzabe, Mandona katika maonyesho ya wiki ya Elimu kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma leo Kulia ni Bibi Agnes Israel. 
 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na wanafunzi na walimu wa shule ya msingi ya  Mungula ya Mkarama,  Singida ambayo inawafundisha watoto wa kabila la Wahadzabe baadaya kufungua maonyesho ya wiki ya Elimu kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma leo.
 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akimsikiza mtoto wa kabila la Wahadzabe,, Kone Paschal wa darasa la kwanza katika shule ya msingi ya Bweni ya Mngulu mkoani Singida katika maonyesho ya wiki ya Elimu kwenye uwanja wa Jamhuri Dodoma leo.
 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda  akipata maelezo kuhusu shughuli mbalimbali zaBritish Coucil wakati alipotembelea banda  la Taasisi hiyo kwenye maonyesho ya Elimu aliyoyafungua kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma leo. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

No comments: