Wednesday, May 6, 2015

WAATHIRIKA WA MVUA MKOA WA MJINI MAGHARIBI WALIVYO FARIJIWA NA WAJUMBE WA SEKREATRIET YA KAMATI MAALUMU YA (NEC) ZANZIBAR.

WAJUMBE wa Sekreatrieti ya Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya (NEC) ya CCM, jana walitembelea maeneno yaliyofikwa na mafuriko ya Mkoa wa Mjini Magharibi kwa lengo la kuangalia na kuwafariji wananchi walioathirika na mkasa huo.



Wakiongozwa na Mwenyekiti wao, ambaye ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Vuai Ali Vuai, wajumbe hao wa Sekreatrieti walitembelea maeneo mbali mbali mkoani humo ikiwemo Mpendae kwa Binti Amrani, Tomondo na Mwanakwerekwe, ambayo yalikumbwa na kadhia hiyo.
Walitumia nafasi hiyo kuwafariji baadhi ya wananchi waliathirika na mafuriko hayo, ambapo baadhi nyumba zimejaa maji na nyengine kuanguka kuta zake, na kusabababisha hasara kubwa.

Wajumbe hao wamewataka wale wote waliokumbwa na janga hilo, kuwa na moyo wa subra na kuiachia Serikali kupitia kitengo cha maafa kutafakari na kuona nini la kufanya. Aidha, wametoa wito na haja kwa jamii nzima ya Wazanzibari kuchukua tahadhari hasa wakati huu wa mvua za masika zinazoendelea kunyesha.

Mvua hiyo kubwa iliyonyesha kwa muda wa masaa matatu mfululizo, kuanzia saa 3:30, iliwafanya wananchi wa Manispaa ya Zanzibar na vVitongoji vyake kushindwa kutekeleza shughuli zao za kimaendeleo.







No comments: