Friday, May 8, 2015

MAFURIKO YAATHIRI DARAJA LA KIKULETWA WILAYANI HAI.

Mvua zinazoendelea kunyesha zimesababisha mafuriko yaliyong'oa miti na kuharibu kingo za daraja la Kikuletwa wilayani Hai.
Mti mkubwa ulizolewa na maji na kisha kugota katika daraja la Kikuletwa.
Baadhi ya wakazi wa Kitongoji cha Kikuletwa wakivuka katika daraja hilo.
Baadhi ya vijana wakiangalia namna ambayo wataweza kuondoa miti hiyo.
Mawe pia katika barabara inayounganishwa na daraja hilo yamezolewa na maji.
Mwenyekiti wa Kijiji cha Chmka Jacob Idd akipita katika daraja hilo kujionea athari za mafuriko hayo.
Baadhi ya wananchi wakitizama eneo ambalo ulikuwepo mti ulisombwa na maji
Miundo mbinu ya maji ya mradi wa Losaa Kia ambao ulikuwa unapeleka maji katika kijiji hicho ikiwa imechukuliwa na maji pia.
Waanchi katika kijiji hicho wakijadili ni cha kufanya.
Wakazi wa maene hayo bado wameendelea kupita katika daraja hilo kwa mashaka.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini 

No comments: