Monday, March 16, 2015

WAHAMIAJI HARAMU 64 RAIA WA ETHIOPIA WAKAMATWA MKOANI DODOMA.

Na. Sylvester Onesmo wa Jeshi la Polisi Dodoma.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma kwa kushirikiana na Wananchi limewakamata Wahamiaji haramu 64  raia wa nchi ya ETHIOPIA (Wahabeshi) katika Kijiji cha KIDOKA, Kata ya KIDOKA, Tarafa ya GOIMA, Wilaya ya na CHEMBA na Mkoa wa DODOMA, mmoja kati yao alikutwa akiwa amefariki dunia aliyetambuliwa kwa jina moja la TAJIRU anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 25 – 30. Watu hao walikuwa wakisafirishwa kwa Lori lenye namba za usajili T.353 AYW Mitsubishi Fuso lililokuwa likiendeshwa na OTHMAN YUNUS MTEKATEKA, miaka 45, na Mkazi wa ILALA Jangwani  jijini Dar es Salaam akitokea Moshi - Kilimanjaro kwenda mkoani Mbeya.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi DAVID MISIME – SACP amesema Mnamo tarehe 14/03/2015 saa 01:00 asubuhi katika kijiji cha KIDOKA walionekana watu wengi wasiofahamika wakiwa wamejificha katika vichaka na mashamba ya watu. 
Watu hao walionekana dhaifu, walikuwa wakila mahindi mabichi na wengine wakiomba kwa wanakijiji waliokuwa wakipita maeneo jirani msaada wa chakula na maji ya kunywa kwa ishara,  kwa kuwa hawakuwa na uwezo wa kuongea lugha ya Kiingereza wala Kiswahili. 

Kamanda MISIME amefafanua zaidi kwa kusema wanakijiji walitoa taarifa kwa uongozi wa kijiji na Jeshi la Polisi, ndipo msako wa kuwakamata ulifanyika na kufanikia kuwakamata watu hao waliotambuliwa kuwa ni raia wa nchi ya ETHIOPIA ambao hawakuwa na vibali vya kuingia/kusafiria. Aidha katika msako huo alikamatwa dereva wa gari hilo aitwaye OTHMAN YUNUS MTEKATEKA, 45yrs na mkazi wa Ilala Jangwani jijini Dar es Salaam na baada ya kuhojiwa alikiri kuwa yeye ndiye aliyekuwa anawasafirisha watu hao akiwa na wenzake wanne ambao walitoweka baada ya gari kuharibika. 

Na kwamba aliwapakia watu hao  tangu tarehe 12/03/2015 huko Moshi – Kilimanjaro kuwapeleka Mkoani Mbeya kwa kupita njia za panya. Baada ya gari kuharibika tarehe 14/03/2015 saa 07:00 usiku katika Kijiji cha Kidoka waliwashusha na kuwapeleka porini kuwaficha kisha kuendelea kutengeneza gari na iliposhindikana waliwatelekeza porini na gari kulitelekeza kijijini.

Kamanda MISIME amewataja wahamiaji haramu hao 63 waliokamatwa kuwa ni:-

1.            FIWADO S/O ERIBALO,

2.            GANOLO S/O ABABA, 15YRS

3.            ABIRIHAM S/ RILE 27YRS

4.            DANIEL S/O AVERA, 25YRS

5.            ARABA S/O LOBE, 18YRS

6.            MEKSO S/O GETACHA, 20YRS

7.            MAMIRIS S/O DANXE, 20YRS

8.            GETACHAM  S/O HAFEBO, 25YRS

9.            MIRATU S/O ABINU, 21YRS

10.         SABSIBE YOHANAS, 18YRS

11.         ABIRIHAMU S/O HADARO, 25YRS

12.         ENDURE S/ SASIE, 18YRS

13.         KABABE S/O WORIW, 22YRS

14.         DANIEL S/O ABARE, 22YRS

15.         ADISE TRAGO, 26YRS

16.         GIRIMA S/O YOHANAS, 19YRS

17.         XILAHUN S/O ABEBE, 18YRS

18.         ESHETU S/O ABEBE, 18YRS

19.         ABEYINE S/O ERTIRO, 26YRS

20.         ENDIRAS S/O MAKANGO

21.         ABABE S/O ACHISO, 30YRS

22.         MISIGUNE S/O DALIKASO, 21YRS

23.         AYANO S/O MALASE, 30YRS

24.         DABADE MISHAMO 30YRS

25.         ERIMIAS S/O ABEBO @ MASORE, 18YRS

26.         ABIRIHAMU S/O ERISIMO, 20YRS

27.         BIRANU S/O ABASE, 25YRS

28.         EYASU S/O BEYENE, 26YRS

29.         KAZALA S/O QADIVE, 2OYRS

30.         ZAKADA S/O GIRIMA, 18YRS

31.         TSAGAYE S/O DESTA, 25YRS

32.         DAGINT S/O URIGO, 34YRS

33.         DAGAZA S/O MOLA, 25YRS

34.         MONAKU S/O ALUMU, 20YRS

35.         ALAMAYU S/O KIZIE, 26YRS

36.         BALAYME S/O WOLDE, 25YRS

37.         ZALALAMU S/O ZAWIDE, 18YRS

38.         FALAKA S/O ELKUCHE, 15YRS

39.         ANA S/O ERSIDO, 27YRS

40.         MALASA S/O TADASA, 22YRS

41.         ASHANAZI S/O MULUNA, 20YRS

42.         ASHANAZI S/O DESTA, 27YRS

43.         SALAMU S/O AYALA, 25YRS

44.         ARABA S/O LUBE, 28YRS

45.         DANIEL S/O TADASA, 22YRS

46.         MANI S/O SALAMU, 24YRS

47.         FANTU S/O LAILA, 28YRS

48.         MANAMU S/O NURYE, 23YRS

49.         NASIRU S/O ANULO, 24YRS

50.         DALALANG S/O ABRA, 20YRS

51.         DELELAG S/O FEKADU, 23YRS

52.         AHMAD S/O ELUSABO, 25YRS

53.         FEKADU S/O ERBALO, 25YRS

54.         GANURO S/O ABEBE, 25YRS

55.         WORKAZAM S/O TIRZE, 28YRS

56.         DANIEL S/O DETEBO, 22YRS

57.         CHARNAT S/O ABEBA, 22YRS

58.         TASHALA S/O BAYENE, 20YRS

59.         ASAUZU S/O DAGAZA, 27YRS

60.         SELAMU S/O WORKUNA, 2OYRS

61.         MEGISO S/O GETACHAU, 2OYRS

62.         TSAUGAYE S/O DETAMO, 15YRS

63.         FANTU S/O TASO, 22YRS.



Uchunguzi zaidi unaendelea ili kuwabaini wahusika wa mtandao huu wa usafirishaji haramu wa binadamu.
Aidha Kamanda MISIME anawashukuru wananchi wakazi wa kijiji cha Kidoka kwa ushirikiano waliouonyesha. Aidha ametoa wito kwa Wananchi kutoa taarifa kwa Jeshi la Polisi na kufichua wahalifu wanaofanya biashara haramu ya usafirishaji haramu wa Binadamu na madereva wasiwe na tamaa mbaya kufanya usafirishaji haramu wa binadamu.



Sehemu ya Wahamiaji haramu 64  raia wa nchi ya ETHIOPIA (Wahabeshi) 

No comments: