Saturday, March 21, 2015

MVUA INAENDELEA KUCHANGAMSHA BAADHI YA MAENEO JIJINI DAR.

Hivi ndivyo hali ilivyo katika maeneo mengi hapa jijini Dar,kutoka na Mvua zinazoendelea kushesha.Kwa Mujibu wa Mamlaka ya Hali ya hewa nchini,inaeleza kwamba Vipindi vya mvua hii inayozidi milimeta 50 ndani ya masaa 24 itaendelea kuwepo katika baadhi ya maeneo ya ukanda wa pwani wa nchi ikihusisha mikoa ya Lindi, Mtwara, Pwani, Dar es Salaam pamoja na kisiwa cha Unguja,hiyo ni kutokana na kuwepo na kuimarika kwa ukanda wa mvua (Inter Tropical Convergency Zone –ITCZ) katika maeneo hayo.
Barabarani huko nako mambo ni kama hivi.
Ndugu zangu hawa ikifika kipindi kama hiki wanakuwa na wakati mgumu kidogo.
Kwa wakazi wa Maeneo ya Mabondeni,wao hawapendi kabisa kipingi hiki.
Mama lishe wakiwa kijiweni kwao kusubiri wateja.
Huku mitaani ndio hakuna kabisa hata kwa kukanyaga,maana ni maji kila kona.
Mdau akikata mtaa.

No comments: