Tuesday, March 10, 2015

MGAWO WA UMEME JIJINI ARUSHA KUMALIZIKA MWEZI JUNI 2015.


Mtaalam kutoka Kampuni ya Sweco International AB, Pal Aberg (kushoto) akiielezea Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini hatua iliyofikiwa ya ujenzi wa kituo cha kupooza na kusambaza umeme cha Njiro kilichopo nje kidogo ya jiji la Arusha.
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini ikiendelea na ziara katika eneo la kituo cha kupooza na kusambaza umeme kilichopo Njiro nje kidogo ya jiji la Arusha.
Mtaalam kutoka Kampuni ya Sweco International AB, Pal Aberg (kulia) akitoa maelezo mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwenye eneo la kituo cha kupooza na kusambaza umeme cha Njiro kilichopo nje kidogo ya jiji la Arusha.
Wataalam kutoka kampuni ya Sweco International AB, wakiendelea na ujenzi katika kituo cha kupooza na kusambaza umeme cha Njiro kilichopo nje kidogo ya jiji la Arusha.
Mtaalam kutoka Kampuni ya Sweco International AB, Pal Aberg (kushoto) akitoa maelezo mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwenye chumba cha kuendesha mitambo ya umeme ( control room) ndani ya kituo cha kupooza na kusambaza umeme kilichopo Njiro nje kidogo ya jiji la Arusha.
Meneja Mradi katika Kituo cha Kupooza na Kusambaza Umeme cha KIA Mhandisi Emmanuel Manirabona (kulia) akiielezea Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini hatua iliyofikiwa ya ujenzi wa kituo hicho kilichopo mkoani Kilimanjaro

No comments: