Tuesday, December 30, 2014

MISS TANZANIA 2014 ASAIDIA KITUO CHA NEW LIFE ORPHANS HOME,BOKO JIJINI DAR.

Miss Tanzania Lilian Kamazima (kulia) akimkabidhi zawadi ya mwaka mpya Msimamizi wa kituo cha kulelea watoto yatima cha New Life kilichopo Boko, Mwanaisha Magambo kwa ajili ya watoto 102 waliopo kituoni hapo, tukio hilo lilifanyika juzi.
Miss Tanzania Lilian Kamazima (kulia) akiwa na Miss Kinondoni Maria Shila wakiwa wamembeba mtoto aliekuwa kwenye kituo cha kulelea watoto yatima cha New Life cha Boko, mtoto huyo alifikishwa hapo akiwa na siku nne tu tangia kuzaliwa kwake.
Sehemu ya Watoto wanaolelewa katika kituo cha kulelea watoto yatima cha New Life kilichopo Boko,wakimsikiliza Miss Tanzania Lilian Kamazima.
Miss Tanzania Lilian Kamazima (kulia) akiwa na watoto katika kituo cha New Life cha Boko.

Redds Miss Tanzania 2014 Lilian Deus Kamazima jumapili iliyopita alitoa misaada ya vyakula vya aina mbalimbali kwa kituo cha New Life Orphans Home kilichopo eneo la Boko nje kidogo ya jiji la D’salaam.

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AAGANA NA MABALOZI WA URUSI, CANADA NA ALGERIA

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Balozi wa Algeria nchini Tanzania, Mhe. Djelloul Tabel, wakati alipofika Ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Desemba 30, 2014 kwa ajili ya kumuaga baada ya kumaliza muda wake wa kazi nchini.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Balozi wa Tanzania nchini Canada, Mhe. Jack Zoka, wakati alipofika Ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Desemba 30, 2014 kwa ajili ya kumuaga akienda kuanza kazi rasmi nchini Canada.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Balozi wa Urusi nchini Tanzania, Mhe. Alexander Rannkikh, wakati alipofika Ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Desemba 30, 2014 kwa ajili ya kumuaga baada ya kumaliza muda wake wa kazi nchini.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Algeria nchini Tanzania, Mhe. Djelloul Tabel, baada ya kumaliza mazungumzo yao yaliyofanyika Ofisini kwa Makamu Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Desemba 30, 2014 alipofika kumuaga baada ya kumaliza muda wake wa kazi nchini.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Canada, Mhe. Jack Zoka, baada ya kumaliza mazungumzo yao yaliyofanyika Ofisini kwa Makamu Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Desemba 30, 2014 alipofika kumuaga akienda kuanza kazi rasmi nchini Canada.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na Balozi wa Urusi nchini Tanzania, Mhe. Alexander Rannkikh, baada ya mazungumzo yao alipofika Ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Desemba 30, 2014 kwa ajili ya kumuaga baada ya kumaliza muda wake wa kazi nchini.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na Balozi wa Tanzania nchini Canada, Mhe. Jack Zoka, baada ya kumaliza mazungumzo yao yaliyofanyika Ofisini kwa Makamu Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Desemba 30, 2014 kwa ajili ya kumuaga akienda kuanza kazi rasmi nchini Canada. Picha na OMR

MWANAFUNZI WA MUCE ALAMBA MIL.3 ZA BAYPORT.

Ruth Bura, Mratibu wa Bima ya Elimu Bayport Tanzania kulia akimkabidhi hundi bwana Kennedy Kaupenda kwa ajili ya kuendelea na masomo ya elimu ya juu baada ya kufariki mzazi wake. 
 
Mratibu wa Bima ya Elimu ya Bayport Tanzania, Ruth Bura kulia, akizungumza jambo katika makabidhiano ya hundi kwa bwana  Kennedy Kaupenda kushoto kwake, Makao Makuu ya Bayport, mapema wiki hii. 

TAASISI ya kifedha ya inayojihusisha na mambo ya mikopo ya Bayport Tanzania, imempatia Sh Milioni tatu (3,000,000) mwanafunzi wa mwaka wa kwanza wa Chuo Kikuu kishiriki cha Mkwawa (MUCE), Kennedy Kaupenda, kufuatia huduma mpya ya Bima ya Elimu inayoendeshwa na taasisi hiyo nchini.

Huduma hiyo mpya ya Bima ya Elimu ya Bayport Tanzania ilianza mapema mwaka huu kwa ajili ya kuwapatia fursa wanafunzi kuendelea na masomo baada ya mzazi aliyejiunga na huduma hiyo kufariki Dunia.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Mratibu wa Bima ya Elimu inayotolewa na Bayport Tanzania, Ruth Bura, alisema Kaupenda alitajwa kama mnufaika kwa mzazi wake aliyefariki Dunia, hivyo waliamua kumtafuta kwa ajili ya kumpatia mafao yake kwa ajili ya kuendelea kupata elimu bila vipingamizi vyovyote.

Alisema huduma hiyo ina vipengele vine ambavyo ni Bronze, Gold, Silver na Exucutive, huku akisema kuwa makato ya kila mwezi ya Bronze ni Sh 2,500, ambapo fao lake ni Sh Milioni 3, wakati makato ya Gold ni Sh 6,250, huku fao lake likiwa ni Sh 7,500,000.

“Pia tunacho kipengele cha Silver ambapo makato yake kwa mwezi ni Sh 3,800, huku mteja akilipwa fao la Sh Milioni 4,500,000 na kipengele cha Executive kikihusisha makato ya Sh 9,000 na kumpatia mteja fao la Sh 10,800,000, huku tukiamini kuwa huduma hii ni sehemu ya kuhakikisha kuwa Watanzania wanawawekea ulinzi wa elimu watoto wao na yoyote wanayemchagua wao,” alisema Ruth.

Akizungumzia fao hilo, Kaupenda alisema hakuwa na imani kuwa angesoma vizuri baada ya baba yake kufariki, ila baada ya kutafutwa na Bayport na kutaarifiwa juu ya mafao hayo, amepata nguvu mpya.

“Nasikitika sana baba kwa kunificha juu ya kujiunga na huduma hii sambamba na kuwa mkopaji wa Bayport, hata hivyo namshukuru kwasababu fedha hizi zimekuja kunipa mwanga mpya wa kuhakikisha kuwa nasoma kwa bidii, nikiamini kiasi cha Sh Milioni tatu kitaniweka katika wakati mzuri mno,” alisema Kaupenda, huku akiwasisitiza wazazi kujiunga kwenye huduma hiyo kwa manufaa ya familia zao.

Mbali na huduma hiyo ya Bima ya Elimu kwa uwapendao, pia Bayport inajihusisha na mikopo kwa watumishi wa umma na kampuni zilizoidhinishwa, ambapo mwishoni mwa mwaka 2014 walizindua huduma ya Mikopo ya Bidhaa, ambapo bidhaa za bodaboda aina ya Lifan, Toyo na Boxer zinakopeshwa kwa wateja wa Bayport Tanzania.


MUSIC PLANET ILIVYO FANA JIJINI DAR.

Wapenzi wa music planet wakipata picha kabla ya kuzama ndani ya Music Planet iliyofanyika Samaki Samaki mpya ya Masaki,jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki iliyoisha.
Masai wakiimba nyimbo zao juu ya mangoma makali kutoka kwa DJ Gabi ikiwa ni mambo ya Music Planet iliyofanyika Samaki Samaki mpya ya Masaki,jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki iliyoisha.
Wapenzi wa Music Planet.
Tequila girl never misses matukio kama haya,ukimsemesha tu anakudunga shot.
Msanii wa Muziki wa Kizazi kipya,Mad Ice akiangusha bonge moja la show sambamba na bendi yake katika Music Planet iliyofanyika Samaki Samaki mpya ya Masaki,jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki iliyoisha.
red carpet smile ndani ya Music Planet.
tabasamu mwanana kwa wadau wakati Music Planet iliyofanyika Samaki Samaki mpya ya Masaki,jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki iliyoisha.
Dj Cartel the undisputed champion 4 rounds wins all by K.O akifanya yake ndani ya Music Planet iliyofanyika Samaki Samaki mpya ya Masaki,jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki iliyoisha.
Mdau Twaba Akiicharaza tumba sambamba na magoma ya DJ Cartel.
Mdau Edward Lusala (kulia) na Mwanamuziki Mad Ice (pili shoto) wakiwa katika picha ya pamoja na wadau walioika kwenye Music Planet iliyofanyika Samaki Samaki mpya ya Masaki,jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki iliyoisha.
Mdau Carlos ambaye ni Mwanzilishi na C.E.O wa Samaki Samaki zote hapa mjini (kulia) akiwa na swaiba wake wa longtime wakienjoy Music Planet iliyofanyika Samaki Samaki mpya ya Masaki,jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki iliyoisha. .
Dj Dully smart on the One n Two.
Tayana (kati) na Mashost zake wakienjoy Music Planet iliyofanyika Samaki Samaki mpya ya Masaki,jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki iliyoisha.

Monday, December 29, 2014

HIVI NDIVYO MVUA ILIVYO LETA ZENGWE LEO JIJINI DAR ES SALAAM.

 Matolori ya kuuzia ice creame yakionekana kununiwa leo,huku wapita njia wakiendelea kupiga mbizi kwenye maji hayo.
 Barabara ya Bibi Titi Mohamed mambo yalikuwa namna hii,wenye magari madogo walipita kwa staili ya maji ya shingo.
 Hapa tena,mwendo wa viatu mkononi.
 Kipando nacho kimeroga.
 Hapa ndio inakuwaga kimbebe,maana daladala ndio lishabuma tena.
 "Hii mvua isharoga tena,na huu mwamvuli miyeyusho kweli".
Hapa dawa ni kutoka nduki tuu...
Kipini cha nguvu barabara ya Umoja wa Mataifa kutokea Faya.

Hakuna namna nyingine ya kuyakwepa maji haya.hapa ni Posta mpya leo.
Posta mpya mambo inogilee.
Mojaaa..... mbiliii.... taaaatuuuuu...... Shtuaaaaa..
Jamaa wakipiga kibeda Nadia iliyobuma katikati ya barabara,maeneo ya Sinza.
Hapa ni Bamaga leo.

SHEIKH ALI MZEE COMORIAN AZIKWA KWENYE MAKABURI YA WANGAZIJA, JIJINI DAR LEO.


 Rais Mstaafu wa awamu ya pili,Alhaj Ali Hassan Mwinyi (wa tatu kushoto),Waziri Mkuu Mstaafu,Dkt. Salim Ahmed Salim (wa nne kulia),Sheik Mkuu wa Tanzania,Shaaban Simba (wa pili kushoto) na Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam,Mussa Salum (wa tatu kulia) wakijumuika pamoja na Waombolezaji wengine kwenye ibada ya Mazishi ya Sheikh Ali Mzee Comorian,katika makaburi ya Wangazija mtaa wa Bibi Titi Mohamed,jijini Dar es salaam mapema leo.Picha zote na Othman Michuzi/Emmanuel Massaka.
Masheikh wakijadiliana jambo kabla ya Mazishi ya Sheikh Ali Mzee Comorian,katika makaburi ya Wangazija mtaa wa Bibi Titi Mohamed,jijini Dar es salaam mapema leo.
Taratibu ya kuandaa Kaburi la Marehemu Sheikh Ali Mzee Comorian zikiendelea katika makaburi ya Wangazija mtaa wa Bibi Titi Mohamed,jijini Dar es salaam mapema leo,huku mvua kubwa ikiendelea kunyesha.
Umati wa Waombolezaji ukiwasili kwenye Makaburi ya Wangazija mtaa wa Bibi Titi Mohamed,jijini Dar es salaam mapema leo,tayari kwa kuhifadhi mwili wa Marehemu Sheikh Ali Mzee Comorian akiefariki Dunia jana.
Sehemu ya Umati wa Waombelezaji ukiwa umebeba Jeneza lenye Mwili wa Marehemu Sheikh Ali Mzee Comorian ukiwasili kwenye Makaburi ya Wangazija mtaa wa Bibi Titi Mohamed,jijini Dar es salaam mapema leo.
Waombolezaji wakiendelea na shughuli ya Mazishi ya Marehemu Sheikh Ali Mzee Comorian kwenye Makaburi ya Wangazija mtaa wa Bibi Titi Mohamed,jijini Dar es salaam mapema leo.
Baada ya mazishi waumini wa Kiislam walifanya zikri kwenye Kaburi la Marehemu Sheikh Ali Mzee Comorian kwenye Makaburi ya Wangazija mtaa wa Bibi Titi Mohamed,jijini Dar es salaam mapema leo.